-
Kamanda Qaani: Uhodari wa utawala wa Kizayuni na Marekani ni kuua wanawake na watoto wasio na hatia
Dec 30, 2023 00:12Brigedia Jenerali Esmail Qaani, Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amehoji, ni mafanikio gani ambayo utawala wa Kizayuni na Marekani zimepata tangu zilipoanzisha vita? na akasema: uhodari wao ni kuua wanawake tu na watoto wasio na hatia.
-
Iran yawanyonga majasusi wanne wa Mossad
Dec 29, 2023 23:15Majasusi wanne waliopatikana na hatia ya kushirikiana na shirika wa kutumia silaha, kutoa vitisho na kushambulia vikosi vya usalama katika mkoa wa kaskazini magharibi wa Azarbaijan Magharibi wamenyongwa siku ya Ijumaa.
-
Khatibu wa Sala ya Ijumaa asisiitiza kudumishwa Hamasa ya tarehe 9 Dey
Dec 29, 2023 08:54Hujjatul-Islam wal-Muslimin Mohammad Javad Haj Ali Akbari, Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran amesisitiza kudumishwa na kuendelezwa kumbukumbu ya Hamasa ya tarehe 9 Dey.
-
Kuuawa shahidi, zawadi ya juhudi kubwa alizofanya Sayyid Razi katika umri wake
Dec 29, 2023 05:07Mazishi ya mwili wa Sayyid Razi Mousavi yalifanyika jana Alhamisi mjini Tehran ambapo umati mkubwa wa wananchi na viongozi wa ngazi za juu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran walihudhuria.
-
Iran: Tuna uwezo wa kupiga nukta yoyote ya Israel wakati wowote tunapopenda
Dec 29, 2023 01:52Mkuu wa Ofisi ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, Iran ina uwezo mkubwa wa kiulinzi kiasi kwamba leo hii inaweza kupiga nukta yoyote ya Israel kwa makombora yanayopiga vizuri mno shabaha, wakati wowote itakapoona kuna haja ya kufanya hivyo.
-
Amir-Abdollahian: Marekani ni kidhabi inapodai haitaki vita vienee; mahandaki ya HAMAS yanafika nje ya Ghaza
Dec 28, 2023 23:41Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, Marekani inaendelea kuusheheneza silaha nzito utawala wa Kizayuni wa Israel bila ya kusita na halafu inadai kuwa eti haitaki vita vya Ghaza vienee nje ya mipaka ya ukanda huo.
-
Hamas yaitaarifu Iran: Tunaweza kukabiliana na Israel Ukanda wa Gaza kwa miezi kadhaa
Dec 28, 2023 22:58Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Hossein Amir-Abdollahian, amesema Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imeifahamisha Jamhuri ya Kiislamu kwamba ina uwezo wa kutosha kuendeleza mapambano na utawala haramu wa Israel katika Ukanda wa Gaza unaozingirwa kwa miaka kadhaa.
-
SEPAH: Kisasi cha mauaji ya Jenerali Razi Mousavi kitakuwa maangamizi kwa Israel
Dec 28, 2023 08:44Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (SEPAH) anasema kuwa, kisasi cha Iran kwa jinai ya utawala wa Kizayuni wa Israel ya kumuua kigaidi mshauri mkuu wa kijeshi nchini Syria hakitakuwa chochote bali ni kuutokomeza kabisa utawala wa Kizayuni unaoikalia kwa mabavu Quds Tukufu.
-
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi kuhusu mtazamo wa kimantiki na wa hoja wa Uislamu kuhusu wanawake
Dec 28, 2023 08:12Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amekutana na maelfu ya wanawake na wasichana na kubainisha mtazamo wa kimantiki na kiakhlaqi wa Uislamu kuhusu nyuga mbalimbali za uwepo wa wanawake katika familia na shughuli zao zisizo na kikomo katika jamii, katika uga wa siasa na katika kusimamia majukumu katika ngazi mbalimbali.
-
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi asalisha Sala ya Maiti ya kuusalia mwili wa Shahidi Mousavi
Dec 28, 2023 03:16Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, leo asubuhi ameongoza Sala ya Maiti ya kuusalia mwili wa Kamanda Shahidi Sayyid Razi Mousavi pamoja na kumsomea Faatiha na kumuombea dua Shahidi huyo.