-
Israel yashambulia ardhi ya Syria baada ya wanamgmabo kuteka Damascus
Dec 08, 2024 10:48Wanajeshi wa utawala ghasibu wa Israel wameanzisha mashambulizi katika ardhi ya Syria na kuingia katika mji wa Quneitra kusini magharibi mwa nchi hiyo karibu na Miinuko ya Golan inayokaliwa kwa mabavu na utawala huo. Uvamizi huo umejiri baada ya makundi ya wanamgambo kuchukua udhibiti wa nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Wanamgambo wa HTS waudhibiti mji wa Damascus huku serikali ya Rais Assad ikianguka
Dec 08, 2024 10:45Serikali ya Syria imeanguka mapema Jumapili katika mwisho wa kushangaza kwa uongozi wa miaka 24 wa Rais Bashar al-Assad katika nchi hiyo ya Kiarabu baada ya kundi la wanamgambo wa Hay’at Tahrir al-Sham (HTS) kuvamia na kuuteka mji mkuu Damascus.
-
Wanamgambo wavamia ubalozi wa Iran nchini Syria baada ya kuanguka serikali ya Assad
Dec 08, 2024 10:41Wanamgambo wanaoungwa mkono na mataifa ya kigeni, wakiongozwa na Hay’at Tahrir al-Sham (HTS), wamevamia ubalozi wa Iran katika mji mkuu wa Syria Damascus baada ya serikali ya Rais Bashar al-Assad kuanguka mapema Jumapili.
-
Israel iliwaua waandishi habari 18 wa Kipalestina mwezi Novemba
Dec 08, 2024 10:38Takriban wafanyakazi 18 wa vyombo vya habari waliuawa mwezi Novemba katika mashambulizi ya nchi kavu na ya anga ya jeshi katili la Israel dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
-
Uungaji mkono wa Marekani kwa sera za kujipanua za Wazayuni
Dec 08, 2024 09:03Sambamba na kukaribia wakati wa kushika rasmi madaraka rais mteule wa Marekani Donald Trump, mipango na njama za Washington za kuunga mkono sera za kujipanua za utawala wa Kizayuni wa Israel nazo pia zimeongezeka.
-
Habari za kutatanisha kuhusu hatima ya Bashar Assad; Ndege ya Assad yatoweka kwenye rada
Dec 08, 2024 03:12Tovuti ya kimataifa ya kufuatilia safari za ndege imeripoti kwamba ndege ambayo huenda ilikuwa imembeba rais wa Syria imetoweka kwenye rada.
-
Reuters: Utawala wa Bashar al-Assad umeanguka, Waziri Mkuu wa Syria: Tuko tayari kukabidhi madaraka
Dec 08, 2024 01:54Shirika la habari la Reuters limenukuu vyanzo vya jeshi la Syria vikisema kuwa maafisa wa ngazi za juu wa jeshi wametangaza kuanguka utawala wa Rais Bashar Assad kwa makamanda wa kijeshi.
-
Iran na Qatar zasisitiza kuimarisha uhusiano
Dec 07, 2024 23:01Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Qatar kwa mara nyingine tena zimesiisitiza azma yao ya kuimarisha na kustawisha zaidi uhusiano wao.
-
Mazungumo ya Astana kuhusu Syria yafanyika Doha Qatar
Dec 07, 2024 23:01Kikao cha Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran, Uturuki na Russia kilifanyika jana Jumamosi katika mji mkuu wa Qatar Doha katika fremu ya kikao cha mchakato wa Astana kwa ajili ya kuupatia ufumbuzi mgogoro wa Syria.
-
WHO: Mashambulizi Kaskazini mwa Gaza yanakwaza ufikishaji wa huduma za afya
Dec 07, 2024 23:00Shirika la Afya la Duniani WHO limetangaza kuwa, mashambulizi ya Israel yanayoendelea Kaskazini mwa Gaza yanaendelea kuzuia ufikishaji wa huduma muhimu za afya zinazohitajika sana.