-
Ulimwengu unasubiri siku ya ghadhabu duniani kuunga mkono wafungwa wa Kipalestina
Jan 26, 2026 23:03Kampeni za kimataifa na za haki za binadamu zimetoa wito kwa watu huru duniani kote kushiriki katika mkusanyiko mkubwa wa kimataifa tarehe 31 Januari kwa ajili ya kuwaunga mkono Wafungwa wa Kipalestina.
-
Kata'ib Hizbullah yatoa wito kwa wanamuqawama kujiandaa kwa 'vita' ili kuinga mkono Iran
Jan 26, 2026 03:06Harakati ya Kata’ib Hizbullah ya Iraq (Brigedi za Hizbullah) imetangaza kuwa iko tayari kushiriki katika vita vyovyote vitakavyotokea ili kuilinda Iran, ikitoa wito kwa wanamapambano duniani kote kujiandaa kwa ajili ya hilo.
-
Bangladesh yalaani India kumruhusu waziri mkuu mtoro Hasina kutoa hotuba ya hadhara
Jan 26, 2026 00:18Bangladesh imesema "imeshangazwa" na "kushtushwa" kuona India imemruhusu waziri mkuu wa zamani mtoro Sheikh Hasina kutoa hotuba ya hadhara mjini New Delhi.
-
Usitishaji vita wa kimaonyesho Gaza; kifuniko cha Wazayuni cha kuendeleza jinai
Jan 25, 2026 08:25Mkurugenzi wa Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa katika maeneo ya Palestina ameonya kuhusu kuendelea kuuawa raia wa Palestina katika Ukanda wa Gaza.
-
Maporomoko ya udongo yaongezeka Indonesia; waokoaji wapambana kunusuru watu waliokwama
Jan 25, 2026 07:49Wafanyakazi wa huduma za uokoaji nchni Indonesia leo wameendelea kufanya juhudi kubwa ndani ya matope kufuatia maporoko ya udongo yaliyoikumba nchi hiyo kwa lengo la kutafuta makumi ya watu ambao hadi sasa bado hawajulikani walipo.
-
Shambulio la droni la Israel laua watoto 2 Gaza
Jan 25, 2026 03:46Watoto wawili wameuawa shahidi katika shambulio la Israel kaskazini mwa Ukanda wa Gaza, katika ukiukaji wa hivi karibuni wa makubaliano ya kusitisha mapigano baina ya utawala huo katili na Harakati ya Muqawama ya Hamas katika eneo hilo la Wapalestina linalokaliwa kwa mabavu.
-
Hizbullah: Tulikwamisha askari 75,000 wa Israel kusini mwa Lebanon
Jan 25, 2026 03:28Katibu Mkuu wa Harakati ya Muqawama ya Hizbullah, Sheikh Naim Qassem amesema wanamapambano wa Muqawama waliwazuia askari 75,000 wa jeshi la adui Mzayuni kusonga mbele kusini mwa Lebanon wakati wa vita vya karibuni zaidi.
-
Amjad Al-Shawa: Watu 18,000 wanahitaji matibabu ya haraka Ukanda wa Gaza
Jan 25, 2026 00:39Mkuu wa shirika lisilo la kiserikali la Palestina huko Gaza ameripoti kuongezeka kwa mgogoro wa kibinadamu katika Ukanda wa Gaza.
-
Bodi ya Amani ya Gaza, jaribio la Trump la kudhoofisha Umoja wa Mataifa
Jan 25, 2026 00:38Tangazo la Marekani la kuunda Bodi ya Amani ya Gaza limeibua wasiwasi mkubwa kuhusu jaribio la Trump la kudhoofisha Umoja wa Mataifa, sambamba na kupeleka mbele ajenda yake binafsi ya kupenda jaha na kujipanua kisiasa.
-
Albanese: Israel ifukuzwe UN kwa kubomoa makao makuu ya UNRWA
Jan 24, 2026 07:03Ripota Maalum wa Umoja wa Mataifa katika maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu ameilaani Israel kwa kubomoa makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Palestina (UNRWA) katika mji wa Baitul Muqaddas Mashariki unaokaliwa kwa mabavu, na kutaka kusimamishiwa unachama utawala huo wa Kizayuni katika Umoja wa Mataifa.