-
Shambulio la droni la Israel laua watoto 2 Gaza
Jan 25, 2026 07:16Watoto wawili wameuawa shahidi katika shambulio la Israel kaskazini mwa Ukanda wa Gaza, katika ukiukaji wa hivi karibuni wa makubaliano ya kusitisha mapigano baina ya utawala huo katili na Harakati ya Muqawama ya Hamas katika eneo hilo la Wapalestina linalokaliwa kwa mabavu.
-
Hizbullah: Tulikwamisha askari 75,000 wa Israel kusini mwa Lebanon
Jan 25, 2026 06:58Katibu Mkuu wa Harakati ya Muqawama ya Hizbullah, Sheikh Naim Qassem amesema wanamapambano wa Muqawama waliwazuia askari 75,000 wa jeshi la adui Mzayuni kusonga mbele kusini mwa Lebanon wakati wa vita vya karibuni zaidi.
-
Amjad Al-Shawa: Watu 18,000 wanahitaji matibabu ya haraka Ukanda wa Gaza
Jan 25, 2026 04:09Mkuu wa shirika lisilo la kiserikali la Palestina huko Gaza ameripoti kuongezeka kwa mgogoro wa kibinadamu katika Ukanda wa Gaza.
-
Bodi ya Amani ya Gaza, jaribio la Trump la kudhoofisha Umoja wa Mataifa
Jan 25, 2026 04:08Tangazo la Marekani la kuunda Bodi ya Amani ya Gaza limeibua wasiwasi mkubwa kuhusu jaribio la Trump la kudhoofisha Umoja wa Mataifa, sambamba na kupeleka mbele ajenda yake binafsi ya kupenda jaha na kujipanua kisiasa.
-
Albanese: Israel ifukuzwe UN kwa kubomoa makao makuu ya UNRWA
Jan 24, 2026 10:33Ripota Maalum wa Umoja wa Mataifa katika maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu ameilaani Israel kwa kubomoa makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Palestina (UNRWA) katika mji wa Baitul Muqaddas Mashariki unaokaliwa kwa mabavu, na kutaka kusimamishiwa unachama utawala huo wa Kizayuni katika Umoja wa Mataifa.
-
Ripoti: Netanyahu hakuenda Davos kutokana na hofu ya kukamatwa
Jan 24, 2026 07:56Vyombo vya habari vya utawala wa Israel vimeripoti kwamba Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, hakuhudhuria Jukwaa la Uchumi Duniani (WEF) mjini Davos wiki hii kutokana na wasiwasi kwamba angeweza kukamatwa nchini Uswisi kufuatia hati ya kukamatwa iliyotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC).
-
Hizbullah: Vitisho vya US dhidi ya Kiongozi Muadhamu vitateketeza eneo lote
Jan 24, 2026 03:31Tawi la Kisiasa la Harakati ya Muqawama ya Hizbullah katika Bunge la Lebanon limeonya kwamba, vitisho vya maneno vya Marekani dhidi ya Iran na Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei vinaweza kushadidisha mvutano katika eneo la Asia Magharibi.
-
Umoja wa Mataifa: Walowezi wa Kizayuni wamewaua Wapalestina 240 Ukingo wa Magharibi
Jan 23, 2026 13:46Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Uratibu wa Masuala ya Kibinadamu (OCHA) imetangaza katika ripoti yake kwamba mwaka jana (2025) walowezi na jeshi la Israel waliua Wapalestina 240 katika Ukingo wa Magharibi.
-
Abdul-Malik Al-Houthi: Baraza la Amani la Trump ni kifuniko tu cha satwa na uporaji
Jan 23, 2026 07:36Sayyed Abdul Malik al-Houthi, kiongozi wa harakati ya Ansarullah ya Yemen amesema kuwa, baadhi ya nchi zinaweka mashinikizo makubwa ya kiuchumi kwa watu wa Yemen kwa kuchelewesha kwa makusudi kuwasili meli na kubainisha kwamba Baraza la Amani la Trump ni kifuniko tu cha satwa na uporaji.
-
Tovuti ya Israel: Ujerumani inaendelea kufadhili mauaji ya kimbari huko Gaza
Jan 23, 2026 03:22Tovuti ya Israel, 972+ imechapisha ripoti ndefu ya uchunguzi kuhusu uhusiano wa kijeshi kati ya Ujerumani na Israel, ikihitimisha kwamba mauzo ya silaha ya Ujerumani yameendelea kumiminika Israel licha ya madai kwamba yamesitishwa kutokana na mauaji ya kimbari ya watu wa Gaza.