-
Makumi wauawa katika shambulio la bomu lililolenga kituo cha treni Pakistani
May 24, 2026 13:11Shambulio la kigaidi katika kituo cha treni katika mji mkuu wa jimbo la Balochistan nchini Pakistani limesababisha vifo vya watu 24 na kujeruhiwa wengine wengi.
-
Israel yawazuia tena Wapalestina wa Gaza kutekeleza ibada ya Hija
May 24, 2026 12:43Watetezi wa haki za binadamu na maafisa wa Palestina wamelaani hatua wanayoieleza kuwa ni kukiuka kwa mfumo uhuru wa ibada, baada ya utawala haramu wa Israel kwa mara nyingine kuzuia maelfu ya Wapalestina wa Gaza kusafiri kwenda Saudi Arabia kwa ajili ya Hija ya kila mwaka.
-
MEE: Misri iliishinikiza Al-Azhar 'kuunga mkono UAE' katika vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran
May 23, 2026 02:43Ripoti zinasema kwamba Ofisi ya Rais wa Misri iliishinikiza taasisi ya Al-Azhar, ambayo ni mamlaka ya juu zaidi ya Waislamu wa madhehebu ya Suni, kuunga mkono hadharani Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na mataifa mengine ya Kiarabu ya Ghuba ya Uajemi katika vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran.
-
Picha za satalaiti zaonyesha uharibifu mkubwa kwenye kambi za kijeshi za Israel kutokana na mashambulizi ya Iran
May 22, 2026 14:53Picha mpya za satalaiti zilizochambuliwa zimefichua uharibifu na hasara kubwa iliyotokea katika vituo vingi vya kijeshi vya Israel kufuatia mashambulizi na operesheni za kujihami za Iran na harakati ya Lebanon Hizbullah na hivyo kuzusha maswali kuhusu ukubwa wa uharibifu ambao Tel Aviv inauficha mbele ya umma.
-
Gaza yaripoti visa zaidi ya 125,000 vya maambukizi yanayohusiana na panya na vimelea: UNRWA
May 22, 2026 06:52Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Palestina (UNRWA) limeripoti visa zaidi ya 125,000 vya maambukizi yanayohusiana na panya na vimelea katika Ukanda wa Gaza ulioathiriwa na vita katika miezi mitano ya kwanza ya mwaka huu.
-
Wanaharakati 87 waliotekwa na vikosi vya Israel waanzisha mgomo wa njaa
May 21, 2026 13:37Angalau wanaharakati 87 waliotekwa nyara na vikosi vya Israel wakati wa uvamizi dhidi ya msafara wa misaada ya kibinadamu kuelekea Gaza, wameanzisha mgomo wa njaa, waandaaji wa safari hiyo walitangaza Jumatano.
-
Israel yavamia meli za Freedom Flotilla na kuwakamata washiriki 100
May 19, 2026 04:00Vyombo vya habari vimeripoti kwamba makomandoo wa jeshi la Wanamaji la Israel wamevamia msafara wa meli za misaada ya kibinadamu kwa ajili ya watu wa Ukanda wa Gaza "Global Sumud Flotilla," ambao ulianza safari Alhamisi iliyopita kutoka Uturuki kuelekea Ukanda wa Gaza.
-
Israel ilianzisha vipi vituo vya kijeshi nchini Iraq na madhara yake ni yapi?
May 18, 2026 16:13Gazeti la Marekani la New York Times limeandika katika ripoti yake kwamba, Israel imeanzisha vituo viwili vya kijeshi vya siri ndani ya ardhi ya Iraq kwa ajili ya kusaidia operesheni zake dhidi ya Iran.
-
Iraq yachora mstari mwekundu; yasema: Ardhi ya nchi hiyo haitatumika kufanya mashambulizi dhidi ya Iran au nchi jirani
May 18, 2026 04:33Iraq imetangaza wazi kuwa kamwe haitaruhusu ardhi yake itumike kwa ajili ya kufanya mashambulizi dhidi ya nchi jirani, hasa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
UN yatoa wito wa kufanyika uchunguzi kuhusu unyanyasaji dhidi ya wafungwa katika magereza ya Israel
May 17, 2026 08:42Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa imelaani ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa na Israel dhidi ya wafungwa wa Kipalestina, ikitaka kufanyike uchunguzi huru, usioegemea upande wowote na wa wazi kuhusu visa vyote vya vifo, mateso, unyanyasaji na ukiukaji mwingine, na kwa wale waliohusika kuwajibishwa.