-
Mabadiliko ya tabianchi; vimbunga vya vumbi vimeathiri watu milioni 330 duniani
Jul 12, 2025 10:39Ripoti mpya ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) imebainisha kuwa, dhoruba za mchanga na vumbi zinaongoza kwa "vifo vya mapema" kutokana na mabadiliko ya tabianchi, ambapo zaidi ya watu milioni 330 katika nchi 150 wameathirika.
-
UNESCO: Mauaji ya wanasayansi wa Iran ni pigo kwa jumuiya ya sayansi duniani
Jul 12, 2025 10:18Katibu Mkuu wa Kamisheni ya Kitaifa ya Iran ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Hassan Fartousi, amesema hujuma za Israel dhidi ya Iran ni tishio kwa "mantiki, sayansi na amani."
-
Pentagon yakiri: Kombora la Iran lilitwanga kambi ya US ya Al-Udeid, Qatar
Jul 12, 2025 08:56Katika pigo kubwa kwa heshima ya kijeshi ya Marekani, Wizara ya Ulinzi ya nchi hiyo (Pentagon) imekiri kwamba, moja ya makombora ya balestiki ya Iran ilipiga moja kwa moja kambi ya anga ya jeshi la US la Al-Udeid nchini Qatar, wakati wa shambulio la kulipiza kisasi la Tehran mwezi uliopita.
-
Gaza inahusiana vipi na janga la Srebrenica?
Jul 12, 2025 06:11Katika mwaka wa 30 wa kumbukumbu ya mauaji ya halaiki ya Srebrenica, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameandika katika ujumbe wake akisema: "Lau dunia ingejifunza kutokana na janga hilo, tusingeshuhudia mauaji mengine ya kimbari dhidi ya Waislamu hii leo, na mara hii huko Gaza."
-
Uhispania na Ireland kujiunga na nchi zaidi ya 20 zitakazochukua 'hatua madhubuti' dhidi ya Israel
Jul 11, 2025 13:15Uhispania na Ireland zitajiunga na zaidi ya nchi 20 zitazokutana katika mji mkuu wa Colombia, Bogota wiki ijayo kutangaza "hatua madhubuti" dhidi ya ukiukaji wa sheria za kimataifa unaofanywa na utawala wa kizayuni wa Israel.
-
IAEA: Baada ya miezi michache, Ujerumani itaweza kuunda silaha za nyuklia
Jul 11, 2025 10:39Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati IAEA Rafael Grossi ametangaza kuwa, Ujerumani inaweza kutengeneza silaha zake za nyuklia ndani ya kipindi cha miezi kadhaa ikiwa itachagua kufanya hivyo. Katika mahojiano na tovuti ya habari ya Poland ya Reczpospolita Grossi amesema Berlin tayari ina nyenzo muhimu za nyuklia, ujuzi na ufikiaji wa teknolojia ya kuunda silaha hizo.
-
Kuhusu vikwazo vya Trump dhidi yake, Albanese asema mwiba wake ‘umechoma ndipo’
Jul 11, 2025 10:14Ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Palestina, Francesca Albanese, amesema hakatishwi tamaa na vikwazo alivyowekewa na Marekani. "Inaonekana mwiba umechoma ndipo," amesema Bi Albanese katika kipindi cha mubashara cha televisheni.
-
Jibu la swali la leo; Kwa nini Ujerumani inataka kuongeza kwa kiasi kikubwa gharama zake za kijeshi?
Jul 11, 2025 04:48Katika hotuba yake kwa bunge la nchi hiyo Bundestag, Kansela wa Ujerumani, Friedrich Merz, sambamba na kuunga mkono ongezeko kubwa la gharama na matumizi ya kijeshi, alisisitiza kuwa anataka kuligeuza jeshi la nchi yake kuwa taasisi ya kupigiwa mfano na inayoongoza katika Shirika la Kijeshi la Nchi za Magharibi (NATO).
-
'Mauaji ya kimbari Gaza ni matokeo ya dunia kushindwa kujifunza kutoka mauaji ya Srebrenica'
Jul 11, 2025 04:11Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesema kuwa iwapo dunia ingezingatia kikamilifu mafunzo kutoka mauaji ya kimbari ya Srebrenica huko Bosnia, basi leo hii tusingeshuhudia jinai nyingine dhidi ya Waislamu, kama inavyotokea Gaza.
-
Unajua kwa nini Marekani imemuwekea vikwazo Ripota Maalumu wa UN kuhusu Maeneo ya Palestina Yanayokaliwa kwa Mabavu?
Jul 10, 2025 22:56Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Marco Rubio, alitangaza Jumatano, Julai 9, kwamba atamuwekea vikwazo Francesca Albanese, Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa katika Maeneo ya Palestina Yanayokaliwa kwa Mabavu, kwa kile alichokiita "juhudi zisizo halali zinazohusiana na uchunguzi wake kuhusu vita vya Israel dhidi ya watu wa Gaza" na eti kwa kuchukua "hatua dhidi ya maafisa wa Marekani na Israel."