-
Rais Maduro wa Venezuela aituhumu WhatsApp kwa kufanya ujasusi
Aug 08, 2024 23:16Rais Nicolas Maduro wa Venezuela ameituhumu WhatsApp kuwa ni mfumo unaofanya ujasusi, na hivyo amewashauri watu kuachana na WhatsApp na kutumia mitandao mingine.
-
UN: Waliowafanyia unyama mahabusu wa Kipalestina katika jela za Israel wawajibishwe
Aug 08, 2024 04:03Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) amesema lazima kuwepo na uwajibishaji dhidi ya ukiukaji wa haki za Wapalestina wanaoshikiliwa katika magereza ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Uingereza katika dimbwi la ghasia za siasa kali za wafuasi wa mrengo wa kulia
Aug 07, 2024 09:20Serikali ya Uingereza imeitisha kikao cha dharura ikiwa ni radiamali ya kuenea ghasia na vitendo vya utumiaji mabavu vya wafuasi wa mrengo wa kulia dhidi ya wahamiaji na Waislamu.
-
NAM: Mauaji ya Ismail Haniyah ni kitendo cha kigaidi
Aug 07, 2024 03:21Harakati ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote (NAM) sanjari na kulaani mauaji ya kigaidi ya Ismail Haniyah, Mkuu wa Kisiasa wa Harakati ya Muqawama ya Palestina HAMAS, imeyataja mauaji hayo kama kitendo cha kigaidi.
-
Umoja wa Mataifa wataka kukabidhiwa madaraka kwa amani nchini Bangladesh
Aug 06, 2024 09:26Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa amesisitiza udharura wa kuhamishwa madaraka kwa njia ya amani nchini Bangladesh, akitoa wito wa kuwajibishwa maafisa wa serikali ya nchi hiyo waliohusika na mauaji ya mamia ya watu na kujeruhiwa maelfu ya waandamanaji katika maandamano ya hivi karibuni dhidi ya serikali.
-
Kuongezeka chuki dhidi ya Uislamu nchini Uingereza
Aug 06, 2024 04:27Taasisi ya Tell Mama inayofuatilia hisia za chuki dhidi ya Uislamu nchini Uingereza kwa mara nyingine tena imehtahadharisha kuhusu vitendo vya kuibua na kutia hofu vinavyofanywa na watu wenye siasa kali za mrengo wa kulia dhidi ya Waislamu nchini humo.
-
Erdogan: Mauaji ya Haniyeh ni kitendo kiovu, mfumo wa dunia umefilisika
Aug 05, 2024 23:27Rais wa Uturuki, Recep Erdogan, alisema jana Jumatatu kwamba mauaji ya kigaidi yaliyofanywa na Israel dhidi ya Ismail Haniyeh, mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas), ni kitendo kiovu ambacho kimetikisa dhamiri za walimwengu, akisisitiza kwamba mfumo wa kimataifa umefilisika mbele ya kile kinachotokea katika Ukanda wa Gaza.
-
Independent: Nini kinatokea Uingereza? Waislamu wanadungwa visu, misikiti imezingirwa
Aug 05, 2024 23:26Gazeti la The Independent linalochalishwa nchini Uingereza limeripoti kuwa ghasia katika miji kama vile Liverpool, Leeds na Belfast ziligeuka kuwa machafuko makubwa mwishoni mwa juma, wakati watu wenye siasa kali za mrengo wa kulia walipopigana na polisi wa kutuliza ghasia, huku kukiripotiwa matukio mengi ya mashambulizi dhidi ya kaumu za waliowachache hususan Waislamu katika mitaa ya miji kadhaa ya nchi hiyo.
-
Waziri Mkuu wa Bangladesh ajiuzulu, akimbia nchi, jeshi kuunda serikali
Aug 05, 2024 09:03Waziri Mkuu wa Bangladesh Sheikh Hasina amejiuzulu na kutoroka nchi huku kukiwa na maandamano makali dhidi ya sera za serikali na utawala wake wa muda mrefu.
-
Machafuko yanaendelea nchini Uingereza
Aug 05, 2024 02:31Miji kadhaa ya Uingereza imekuwa uwanja wa ghasia za mitaani na makabiliano kati ya polisi na wafuasi wa makundi ya mrengo wa kulia na vile vile wapinzani na watu wenye chuki dhidi ya wahajiri wa Kiiislamu.