Mazungumzo ya kitaifa DRC: Masharti ya Rais Tshisekedi yaibua hisia mseto
-
Mazungumzo ya kitaifa DRC: Masharti ya Rais Tshisekedi yaibua hisia mseto
Siku moja baada ya mfumo uliowekwa na rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa ajili ya mazungumzo ya kitaifa yaliyoitishwa na sehemu ya upinzani na kuhimizwa na washirika kadhaa wa Magharibi wa DRC kutatua mgogoro unaosambaratisha mashariki mwa nchi, wengi mjini Kinshasa wametoa hisia zao.
Katika hotuba yake ya Mwaka Mpya kwa wanadiplomasia huko Kinshasa, Januari 31, Rais Félix Tshisekedi alielezea mistari myekundu ya mazungumzo ya kitaifa yanayokusudiwa kusaidia nchi hiyo kutoka kwenye mgogoro katika mikoa ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini.
Rais Felix Tshisekedi pia alidai kwamba mchakato huo ufanyike ndani ya mfumo mkali, yaani kwamba ufanyike katika eneo la kitaifa na chini ya udhibiti wa taasisi, bila kupinga utawala au maamuzi ya mahakama ambayo yamefanywa hadi sasa. Hatua hii ya mwisho inakuja wakati viongozi kadhaa wa AFC/M23, pamoja na rais wa zamani Joseph Kabila, wamehukumiwa adhabu ya kifo, na baadhi ya wapinzani wanaishi uhamishoni.
Matamshi haya yameibua hisia nyingi na tofauti jijini Kinshasa. Mwitikio unaotarajiwa sana kutoka kwa Kanisa Katoliki, ambalo linatoa upatanishi wake pamoja na madhehebu mengine ya kidini katika mzozo unaoigawanya mashariki mwa DRC, unaangaliwa kwa makini.
Kwa upande mwingine, matamshi ni makali zaidi kutoka kwa muungano wa rais wa zamani Joseph Kabila. Ferdinand Kambere, naibu katibu wa kudumu wa chama tawala cha zamani, anasisitiza juu serikali kubadilika kwa kauli zake na kutaka kuleta masharti yasiyo kuwa na msingi.