Wanajeshi kadhaa wauawa kaskazini mashariki mwa Libya
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i13732-wanajeshi_kadhaa_wauawa_kaskazini_mashariki_mwa_libya
Vyombo vya habari vya nchi za Kiarabu vimeripoti habari ya kuuawa wanajeshi kadhaa wa Jenerali Khalifa Haftar katika mripuko wa bomu uliotokea kaskazini mashariki mwa Libya.
(last modified 2026-01-14T08:12:18+00:00 )
Aug 21, 2016 23:28 UTC
  • Wanajeshi kadhaa wauawa kaskazini mashariki mwa Libya

Vyombo vya habari vya nchi za Kiarabu vimeripoti habari ya kuuawa wanajeshi kadhaa wa Jenerali Khalifa Haftar katika mripuko wa bomu uliotokea kaskazini mashariki mwa Libya.

Duru hizo zimeripoti kuwa wanajeshi sita wa Jenerali Mstaafu Khalifa Haftar ambaye anahesabiwa kuu ndiye mkuu wa jeshi katika eneo la mashariki mwa Libya waliuawa jana baada ya kutokea mripuko wa bomu katika eneo la Guwarsha, magharibi mwa Benghazi.

Jenerali Mstaafu, Khalifa Haftar

 

Jumanne iliyopita pia, Baraza la Wafanyamapinduzi la Benghazi lilitangaza kuwa, wanajeshi 38 wa Khalifa Haftar wameuawa katika mapigano na askari wa baraza hilo, huko mashariki mwa Libya.