Vikosi vitiifu kwa Jenerali Haftar vyashambulia bandari za mafuta Libya
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i15124-vikosi_vitiifu_kwa_jenerali_haftar_vyashambulia_bandari_za_mafuta_libya
Vikosi vitiifu kwa Jenerali Khalifa Haftar kamanda wa kijeshi wa mashariki mwa Libya vimezishambulia bandari za mafuta nchini humo na kukabiliana na walinzi wa vituo hivyo.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Sep 11, 2016 09:43 UTC
  • Vikosi vitiifu kwa Jenerali Haftar vyashambulia bandari za mafuta Libya

Vikosi vitiifu kwa Jenerali Khalifa Haftar kamanda wa kijeshi wa mashariki mwa Libya vimezishambulia bandari za mafuta nchini humo na kukabiliana na walinzi wa vituo hivyo.

Ali al Hassi Msemaji wa Petrol Facilities Guard (PFG) katika bandari hizo za mafuta ameeleza kuwa vikosi vitiifu kwa Jenerali Haftar vimezishambulia bandari za Zuweitina, Ras Lanuf na al Sidra mashariki mwa mji wa Sirte na kuushambulia pia mji wa karibu wa Ajdabiya na kusababisha mapigano. Mhandisi mmoja wa masuala ya bandari amethibitisha kujiri mashambulizi hayo ya vikosi vya Haftar na kueleza kuwa moja ya matanki ya kuhifadhia mafuta katika bandari ya a Sidra limechomwa moto kwenye makabiliano. Huku hayo yakiripotiwa Shirika la Habari la LANA lenye mfungamano na bunge la Libya linalotambuliwa kimataifa limemnukuu Kanali Ahmad Mesmari akisema leo kuwa, vikosi vitiifu kwa Jenerali Khalifa Haftar hivi sasa vinadhibiti bandari hizo tatu huko Sirte.

Bandari tatu za mafuta za al Zuweitina, al Sidra na Ras Lanuf zilizoshambuliwa na vikosi vya Jenerali Haftar nchini Libya