Watu 24 wapoteza maisha katika maporomoko ya ardhi Kenya
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i57448-watu_24_wapoteza_maisha_katika_maporomoko_ya_ardhi_kenya
Watu wasiopungua 24 wamepoteza maisha magharibi mwa Kenya kufuatia maporomoko ya ardhi katika Kaunti ya West Pokot.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Nov 23, 2019 09:44 UTC
  • Watu 24 wapoteza maisha katika maporomoko ya ardhi Kenya

Watu wasiopungua 24 wamepoteza maisha magharibi mwa Kenya kufuatia maporomoko ya ardhi katika Kaunti ya West Pokot.

Kwa mujibu wa Kamishna wa Kaunti ya West Pokot, Apollo Okello, tayari wameshapata miili ya watu 12 wakiwemo watoto saba baada ya maporomoko makubwa ya ardhi kukumba vijiji vya Nyarkuliana na Parua Ijumaa usiku kufuatia mvua kubwa ambazo zilinyesha kwa masaa kadhaa. Amesema kunaendelezwa oparesheni za kutafuta miili ya waathirika wa tukio hilo. Mvua hizo aidha zimesebabisha kufungwa sehemu moja ya barabara ya Kitale-Lodwar karibu na Ortum na hivyo kuathiri vibaya shughuli za uokoaji.

Barabra ya  Kitale-Lodwar nchini Kenya

Aidha Daraja la Muruny katika eneo hilo limesombwa na mafuriko kufuatia mvua hizo.

Mvua kubwa zimekuwa zikinyesha kote Kenya katika wiki za hivi karibuni na kusababisha hasara kubwa.

Mwezi Aprili mwaka 2018, watu 100 walipoteza maisha kufuatia maporomoko ya ardhi katika maeneo kadhaa ya Kenya huku maelfu wakipoteza makao.