-
Eswatini ilipokea hongo ya dola milioni 5 kutoka Marekani ili kukubali wahamiaji waliotimuliwa
Nov 19, 2025 23:26Eswatini imethibitisha kupokea dola milioni 5.1 kutoka Washington kama sehemu ya makubaliano ya kupokea wahamiaji waliofukuzwa Marekani licha ya kutokuwa na uhusiano wowote na taifa hilo la kusini mwa Afrika.
-
Katibu Mkuu wa UN: Ugaidi katika eneo la Sahel ni tishio linaloongezeka
Nov 19, 2025 09:05Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amewatahadharisha viongozi duniani kwamba ugaidi katika eneo la Sahel barani Afrika ni tishio linaloongezeka duniani.
-
Rais wa Nigeria athibitisha kuuawa afisa wa ngazi ya juu wa jeshi
Nov 19, 2025 08:54Rais wa Nigeria amethibitisha kuwa Brigedia jenerali Musa Uba ameuawa na kundi la kigaidi akiwa matekani. Mauaji hayo yamefanywa siku chache baada ya afisa huyo wa ngazi ya juu wa jeshi la Nigeria kutekwa nyara na wanamgambo wa kundi la ISWAP kufuatia shambulio la kuvizia kaskazini mashariki mwa Jimbo la Borno ambalo pia liliwaua wanajeshi wanne.
-
Rais Samia: Ghasia za uchaguzi zinaweza kuathiri upatikanaji wa fedha
Nov 19, 2025 03:28Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania jana alisema kuwa ghasia zilizotokea baada ya uchaguzi wa Oktoba 29 zinaweza kuathiri upatikanaji wa ufadhili wa kimataifa kwa nchi hiyo.
-
Onyo la Afrika Kusini kuhusu njama ya kuwahamisha Wapalestina kwa nguvu
Nov 18, 2025 22:54Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini, Ronald Lamola, amesema kuwasili Johannesburg wiki iliyopita kwa ndege iliyobeba wakimbizi wa Kipalestina ni “operesheni iliyopangwa waziwazi” ya kuwahamisha Wapalestina.
-
Mkuu wa jeshi la Nigeria aagiza kutafutwa usiku na mchana mabinti wa shule waliotekwa nyara
Nov 18, 2025 22:53Jenerali wa ngazi ya juu wa jeshi la Nigeria ameviagiza vikosi vya jeshi hilo kuendesha msako wa "usiku na mchana" ili kuwanusuru mabinti 25 wa shule waliotekwa nyara kaskazini-magharibi mwa nchi hiyo.
-
Kwa nini Afrika Kusini imedhamiria kufuatilia kesi ya mauaji ya halaiki huko Gaza?
Nov 18, 2025 22:42Serikali ya Afrika Kusini imetangaza kuwa, itaendelea kuchukua hatua za kisheria dhidi ya Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) kwa tuhuma za kutenda mauaji ya kimbari katika Ukanda wa Gaza.
-
Wagonjwa ni kati ya watu karibu 30 waliouawa katika shambulio la waasi mashariki mwa Kongo
Nov 18, 2025 07:28Takriban watu 29, wakiwemo wagonjwa wameuawa katika shambulio linalodaiwa kufanywa na waasi wa Allied Democratic Forces (ADF) ambalo lililenga kituo cha afya na vijiji kadhaa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Jeshi la Sudan laondoka "Umm Sayala" huku mapigano makali yakiendelea Kordofan
Nov 18, 2025 03:36Chanzo cha kijeshi kimethibitisha kwamba jeshi la Sudan na vikosi washirika jana Jumatatu viliondoka katika mji wa Umm Sayala huko Darfur Kaskazini, saa chache baada ya kuukomboa kutoka kwa wapiganaji wa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), huku mapigano yakiiendelea katika maeneo kadhaa ya eneo hilo.
-
Nchi za Maziwa Makuu zaitangaza RSF kuwa ni kundi la kigaidi
Nov 17, 2025 22:52Wizara ya Mambo ya Nje ya Sudan imetangaza kwamba Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Maziwa Makuu uliofanyika Kinshasa mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo umeidhinisha pendekezo la kuvitangaza Vikosi vya Msaada wa Haraka RSF kuwa ni "kundi la kigaidi."