-
"Hali ngumu" ya utawala wa Kizayuni katika vita na Hizbullah ya Lebanon
Feb 22, 2024 06:42Vyanzo vya habari vya Kiebrania vimeonya juu ya hali ngumu itakayoikabili Israeli ikiwa itaanzisha vita dhidi ya Lebanon na uwezekano wa kuangamia maelfu ya Waisraeli, kufuatia vitisho vya mara kwa mara vya maafisa wa Israeli dhidi ya Lebanon na Hizbullah.
-
Rais wa Brazil afananisha jinai za Israel na zile za Hitler wa Ujerumani
Feb 21, 2024 23:09Jinai zinazofanywa na Israel dhidi ya Wapalestina huko Gaza zinahesabiwa kuwa kubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa katika miongo ya karibuni na aghalabu ya jinai hizo zimetajwa kuwa ni maangamizi ya kizazi huku zikilinganishwa na uhalifu ulizofanywa na Adolf Hitler, kiongozi Manazi wa Ujerumani, katika Vita vya Pili vya Dunia.
-
Radiamali zilizotolewa dhidi ya kura ya veto ya Marekani ya kupinga rasimu ya Azimio la Baraza la Usalama la kusitisha mapigano Ghaza
Feb 21, 2024 05:38Kutumia Marekani kura ya turufu dhidi ya rasimu ya Azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa la kusitisha mapigano Gaza kumekabiliwa na radiamali na mijibizo ya shakhsia na viongozi wengi duniani.
-
Matukio ya Magharibi mwa Asia; ajenda kuu ya mazungumzo ya Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran na Saudi Arabia
Feb 20, 2024 22:48Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Saudi Arabia wamejadili kuhusu matukio ya kieneo na kimataifa, vikiwemo vita vya Gaza na kuimarisha uhusiano wa simu.
-
Kuanza kusikilizwa na ICJ shauri kuhusu Israel kukalia kwa mabavu ardhi za Palestina
Feb 20, 2024 03:15Jumatatu ya jana tarehe 24 Februari 2024, Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ), ilianza kusikiliza shauri la kihistoria la kuamua kuhusu uhalali wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel wa kuzivamia na kuzikalia kwa mabavu ardhi za Palestina.
-
Mamlaka ya Palestina: Hamas ni sehemu muhimu ya medani ya siasa ya Palestina
Feb 19, 2024 22:53Waziri Mkuu wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina amesisitiza kuwa, Harakati ya Mambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) ni sehemu muhimu ya uwanja wa kisiasa wa Palestina.
-
Kulaaniwa utawala wa Kizayuni wa Israel katika mkutano wa Umoja wa Afrika
Feb 19, 2024 04:47Viongozi wa nchi za Kiafrika waliokutana mjini Addis Ababa, mji mkuu wa Ethiopia, wamelaani jinai zinazofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel huko Gaza na kutoa wito wa kusitishwa mara moja mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina.
-
Kuzinduliwa mifumo mipya ya makombora nchini Iran
Feb 19, 2024 01:03Katika kuendelea ustawi wa Jamhuri ya Kiislamu katika sekta ya makombora, mifumo dhidi ya makombora ya balestiki kwa jina la "Arman", na mfumo wa ulinzi wa anga ya juu wa Azarkhash, ambao uliundwa kwa juhudi za wataalamu wa Wizara ya Ulinzi ya Iran ulizinduliwa juzi Jumamosi.
-
Vitisho vipya vya wakosoaji wa Natenyahu; Kuvunjwa Baraza la Mawaziri la Vita
Feb 18, 2024 06:02Sambamba na Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni Benjamin Netanyahu kuendeleza tabia yake ya kujichukulia hatua za upande mmoja, wakosoaji wake wametishia kulivunja Baraza la Mawaziri la Vita la utawala huo.
-
Kuongezeka kasi ya kuachana na matumizi ya dola kwa wanachama wa kundi la BRICS
Feb 17, 2024 23:29Russia, China na India ambazo ni wanachama wa kundi la BRICS zimepunguza matumizi ya dola ya Marekani katika biashara zao kwa asilimia 95 kufuatia kuendelea mchakato wa kutupilia mbali matumizi ya sarafu ya hiyo ya Marekani.