Rais Rouhani: Matatizo ya mazingira yatatuliwe kimataifa
https://parstoday.ir/sw/news/iran-i31282-rais_rouhani_matatizo_ya_mazingira_yatatuliwe_kimataifa
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema ulindaji mazingira ni dharura kwa ajili ya afya, ustawi na kuzuia kuhajiri watu kutoka maeneo yao.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Jul 03, 2017 03:41 UTC
  • Rais Rouhani: Matatizo ya mazingira yatatuliwe kimataifa

Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema ulindaji mazingira ni dharura kwa ajili ya afya, ustawi na kuzuia kuhajiri watu kutoka maeneo yao.

Aidha amesisitiza kuwa, utatuzi wa tatizo la mazingira ni jambo linalohitaji uwekezaji, mikakati maalumu na ushirikiano wa kieneo na kimataifa.

Rais Hassan Rouhani ameyasema hayo leo Jumatatu mjini Tehran katika mkutano wa kimataifa wa "Kukabiliana na Kimbunga cha Mchanga, Changamoto na Njia za Kivitendo za Utatuzi." Ameongeza kuwa, asilimia 80 ya kimbunga cha mchanga nchini Iran hutokana na uharibifu wa mazingira katika nchi  za  Iraq, Jordan, Kuwait, Syria, Saudi Arabia, Pakistan, Afghanistan na Turkmenistan.

Rais Rouhani akihutubu mkutano wa mazingira Tehran

Kwingineko, katika hotuba yake, Rais Rouhani amesema, ugaidi ni sumu ambayo imeteka eneo lote la Mashariki ya Kati na kwamba tawala zote zinazotumia ugaidi kufikia malengo haramu zifahamau ugaidi pia utazisibu.

Wakati huo huo mshauri wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akizungumza katika kongamano hilo, ameipongeza Iran kwa hatua ilizochukua kukabiliana na uchafuzi wa mazingira.