-
Kiongozi wa Wademocrat katika Bunge la US: Trump anasema uwongo kuhusu Iran
Feb 25, 2026 03:30Kiongozi wa wabunge wa chama cha Democratic katika Baraza la Wawakilishi la Marekani amesema, Rais wa Marekani Donald Trump anasema uwongo kuhusu Iran.
-
Al-Burhan atoa fursa ya msamaha kwa wapiganaji wa RSF watakaoweka silaha zao chini
Feb 25, 2026 03:29Mwenyekiti wa Baraza la Utawala la Sudan, Abdel Fattah al-Burhan, ametangaza fursa ya msamaha kwa wapiganaji wa Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF) ikiwa wataweka silaha zao chini.
-
Afisa mwandamizi wa PLO asema, HAMAS si kundi la kigaidi, apinga mpango wa kuipokonya silaha
Feb 25, 2026 03:28Katibu Mkuu wa Kamati ya Utendaji ya Chama cha Ukombozi wa Palestina (PLO), Azzam al-Ahmad amesema, Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS si shirika la kigaidi na ameukataa wito wa kupokonywa silaha zake huku akibainisha kuwepo mipango ya kufanya mazungumzo kuhusu uwezekano wa harakati hiyo kujumuishwa katika PLO.
-
UN yatoa wito wa msaada wa dharura kwa wakimbizi wa Burundi waliopo na wanaorudi nchini
Feb 25, 2026 03:28Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, (UNHCR) limetangaza kuwa, ufadhili endelevu na wa uhakika unahitajka ili kuendeleza ulinzi kwa wakimbizi na kusaidia urejeaji na ujumuishaji wa raia wanaorudi nchini Burundi, wakati huu ambapo kambi zinzowahifadhi zinakabiliwa na msongamano mkubwa na uhaba wa huduma muhimu.
-
Takriban watu milioni 6.5 wanakabiliwa na njaa kali kutokana na ukame ulioikumba Somalia
Feb 25, 2026 00:57Serikali ya Somalia na Umoja wa Mataifa zimetangaza kuwa wananchi wa Somalia wasiopungua milioni 6.5 wanakabiliwa na njaa kali kutokana na ukame ulioiathiri nchi hiyo.
-
Mohajerani: Iran inafadhilisha diplomasia badala ya vita
Feb 24, 2026 22:57Msemaji wa serikali ya Iran amesema, Jamhuri ya Kiislamu inafadhilisha diplomasia kuliko vita, lakini inaviona viwili hivyo kama mikakati ya kulinda maslahi ya taifa la Iran.
-
Ripoti: Israel iliwamiminia risasi, kuwaua wafanyakazi wa misaada Tel al Sultan, Gaza
Feb 24, 2026 22:56Karibu risasi elfu moja zilifyatuliwa na wanajeshi wa Israel katika mauaji ya kiholela dhidi ya wafanyakazi wa misaada huko Tel al-Sultan, Gaza, huku baadhi yao wakiuawa kwa kupigwa risasi kwa karibu, kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa hivi karibuni.
-
Msemaji wa M23 auawa katika shambulio la droni mashariki mwa DRC
Feb 24, 2026 22:54Msemaji wa waasi wa M23 ameripotiwa kuuawa katika shambulio la ndege isiyo na rubani mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Madagascar: Ushirikiano wetu na BRICS utatupa fursa mpya
Feb 24, 2026 22:54Rais wa mpito wa Madagascar, Michael Randrianirina amesema kwamba, nchi hiyo inatazama ushirikiano na jumuya ya BRICS kama njia ya kuelekea kwenye fursa mpya za kiuchumi na ushirikiano wa kimataifa.
-
Jibu kali la Iran kwa hatua ya Umoja wa Ulaya dhidi ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Feb 24, 2026 22:53Katika kujibu hatua haramu ya Umoja wa Ulaya dhidi ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeyataja majeshi ya majini na anga ya nchi zote wanachama wa umoja huo kuwa mashirika ya kigaidi.