-
Mkuu wa jeshi la Pakistan azungumza kwa kina na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran mjini Tehran
May 23, 2026 12:35Asim Munir, Mkuu wa jeshi la Pakistan amefanya mazungumzo ya muda mrefu na Waziri wa Mambo ya Nje Abbas Araqchi mjini Tehran, huku jitihada za kidiplomasia zikishika kasi ili kuzuia kushtadi hali ya mgogoro katika Asia Magharibi.
-
Iran yaiambia UN: Nchi za Ghuba ya Uajemi zinapasa kutoa jibu na kulipa fidia kwa mchango wao katika vita vya Marekani na Israel
May 23, 2026 12:32Amir Saeid Iravani Balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa nchi za kusini mwa Ghuba ya Uajemi na Jordan zinabeba dhima ya kuzisaidia Marekani na Israel katika uvamizi wao dhidi ya Iran.
-
Kamanda Talaei-Nik: Trump hana chaguo ila kukubali haki ya Iran
May 23, 2026 12:29Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Iran amesema: "Kushindwa adui kufungamana na matakwa halali ya taifa la Iran kutasababisha gharama kubwa na kushindwa zaidi adui Mzayuni na Marekani."
-
Kundi la Kimataifa la Mawasiliano lazitaka pande hasimu Kongo kufanikisha juhudi za kukabiliana na Ebola
May 23, 2026 12:26Kundi la Kimataifa la Mawasiliano la Eneo la Maziwa Makuu (ICG) limebainisha wasiwasi wake kuhusu kuendelea mzozo mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo huku nchi hiyo ikiwa imeathiriwa na mlipuko wa ugonjwa hatari wa Ebola.
-
Kwa nini mashambulizi dhidi ya wageni yanaongezeka Afrika Kusini?
May 23, 2026 12:20Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch (HRW) limeonya kuhusu wimbi jipya la mashambulizi ya chuki dhidi ya wageni nchini Afrika Kusini huku makundi yanayopinga wahamiaji na wageni nchini humo yakiendelea kuandamana na kushajiiisha vitendo vya kuwalenga raia wa kigeni wakiwemo Wazimbabwe.
-
Hukumu za Ibada ya Hija- Ihram
May 23, 2026 08:06Baada ya miaka mingi na kuwa mbali na Makka, Mtume Muhammad (saw) na Masahaba wake walielekea katika eneo hilo kwa ajili ya kufanya ibada ya Umra katika mwaka wa 6 wa Hijria. Wote walivaa Ihram mahali paitwapo Dhul-Hulaifah (Msikiti Shajara), ambapo palikuwa umbali wa kilomita 450 kutoka Makka.
-
Rais Pezeshkian awataka wataalamu wa mahusiano ya umma kuvunja vikwazo vya vyombo vya habari vya Kizayuni
May 23, 2026 03:05Rais Masoud Pezeshkian anasema wataalamu wa mahusiano ya umma wanapaswa kuchukua jukumu muhimu katika kuongeza uelewa wa umma, ikizingatiwa kwamba vyombo vya habari vya Kizayuni vinawazuia watu kuona na kujua ukweli.
-
Mkuu wa ujasusi wa Trump ajiuzulu kwa mashinikizo ya White House kuhusu vita haramu dhidi ya Iran
May 23, 2026 03:01Mkurugenzi wa Ujasusi wa Kitaifa (DNI) wa Rais wa Marekani, Donald Trump, Tulsi Gabbard, amejiuzulu kutokana na shinikizo kubwa la Ikulu ya White House baada ya kupinga vikali vita haramu na vya uchokozi vya Marekani dhidi ya Iran.
-
MEE: Misri iliishinikiza Al-Azhar 'kuunga mkono UAE' katika vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran
May 23, 2026 02:43Ripoti zinasema kwamba Ofisi ya Rais wa Misri iliishinikiza taasisi ya Al-Azhar, ambayo ni mamlaka ya juu zaidi ya Waislamu wa madhehebu ya Suni, kuunga mkono hadharani Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na mataifa mengine ya Kiarabu ya Ghuba ya Uajemi katika vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran.
-
Baqaei: Kuharibiwa Taasisi ya Pasteur ya Iran ni tishio kwa usalama wa afya wa kikanda
May 23, 2026 02:41Ismail Baqaei, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, amechapisha nukuu ya ripoti ya jarida la masuala ya tiba la The Lancet kuhusu uharibifu uliosababishwa na mashambulizi ya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel kwenye Taasisi ya Pasteur ya Iran, na kusisitiza kwamba kuharibiwa taasisi hiyo ni tishio kwa usalama wa kikanda.