Kwa nini mashambulizi dhidi ya wageni yanaongezeka Afrika Kusini?
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i138570-kwa_nini_mashambulizi_dhidi_ya_wageni_yanaongezeka_afrika_kusini
Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch (HRW) limeonya kuhusu wimbi jipya la mashambulizi ya chuki dhidi ya wageni nchini Afrika Kusini huku makundi yanayopinga wahamiaji na wageni nchini humo yakiendelea kuandamana na kushajiiisha vitendo vya kuwalenga raia wa kigeni wakiwemo Wazimbabwe.
(last modified 2026-05-23T12:25:56+00:00 )
May 23, 2026 12:20 UTC
  • Chuki dhidi ya wageni Afrika Kusini
    Chuki dhidi ya wageni Afrika Kusini

Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch (HRW) limeonya kuhusu wimbi jipya la mashambulizi ya chuki dhidi ya wageni nchini Afrika Kusini huku makundi yanayopinga wahamiaji na wageni nchini humo yakiendelea kuandamana na kushajiiisha vitendo vya kuwalenga raia wa kigeni wakiwemo Wazimbabwe.

Indhari hii imetolewa katika ripoti Jumanne iliyopita huku kukiwa na ongezeko la maandamano katika miji ya Afrika Kusini, ikiwemo Johannesburg, Pretoria na Durban.

Makundi kama vile 'March and March' na 'Operation Dudula'; makundi mawili yanayopinga wahamiaji nchini Afrika Kusini  yamekuwa yakichochea hatua kali dhidi ya wahamiaji wasio na hati za kuishi nchini humo. Makundi hayo yanatajwa kuongoza maandamano katika miji kadhaa nchini Afrika Kusini.

"Tunaendelea kupokea ripoti kupitia mitandao yetu ya kijamii kuhusu vitisho, vitisho, unyanyasaji, kufukuzwa kinyume cha sheria, ubaguzi mahali pa kazi, unyang'anyi wa polisi, na kunyimwa huduma za afya na huduma nyingine za kimsingi zinazoathiri wahamiaji na wakimbizi," ameema Mike Ndlovu, mratibu wa vyombo vya habari wa Kopanang Africa Against Xenophobia (KAAX).

"Aina za kawaida za madhara ni pamoja na unyanyasaji kupitia matamshi kama kutukanywa, kudhalilishwa, kufukuzwa, ubaguzi katika kliniki na sehemu za kazi, kunyang'anywa bidhaa na katika baadhi ya matukio kushambuliwa kimwili," Ameweka wazi Ndlovu alipohojiwa na televisheni ya al Jazeera.