-
Iraq yamueleza mjumbe wa Marekani: Uundaji wa serikali ni 'suala letu la ndani'
Feb 24, 2026 08:22Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq, Fuad Hussein amesema, uundaji wa serikali mpya ya nchi hiyo ni "suala la ndani," ukiwa ni mjibizo uliotolewa wiki chache baada ya Marekani kutishia kufuta msaada na uungaji mkono wake kwa nchi hiyo ya Asia Magharibi.
-
Israel imepeleka Ghaza maboksi yenye mafuvu na miili iliyonyofolewa ya wanawake Wapalestina
Feb 24, 2026 07:45Mbunge wa kujitegemea, ambaye pia ni kiongozi wa zamani wa chama cha Leba nchini Uingereza Jeremy Corbyn, ametoa simulizi za kutisha zilizotokana na maelezo ya mkurugenzi wa Hospitali ya Al-Shifa katika Ukanda wa Ghaza uliozingirwa, zinazobainisha kwa undani jinsi utawala wa kizayuni wa Israel ulivyopeleka katika eneo hilo masanduku kadhaa yenye mafuvu ya vichwa na mabaki ya Wapalestina yaliyokatwakatwa.
-
Mwana wa Rais wa Uganda amuita 'Hitler' kiongozi wa RSF aliyekutana na baba yake hivi karibuni
Feb 24, 2026 07:43Mwana mtatanishi wa Rais wa Uganda Yoweri Museveni ambaye ni mkuu wa majeshi ya nchi hiyo Muhoozi Kainerugaba ametoa matamshi yasiyo ya kawaida katika kumshambulia kiongozi wa wanamgambo wa Sudan wa Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF), Mohamed Hamdan Dagalo ambaye hivi karibuni alikutana na baba yake huko nchini Uganda.
-
Netanyahu kuunda 'muungano' utakaoshirikisha Waarabu kukabiliana na mihimili ya Sunni na Shia
Feb 24, 2026 07:42Waziri mkuu wa utawala wa kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu amesema juhudi zinaendelea kufanywa za kuunda kile alichokielezea kama "muungano" wa kikanda wa kukabiliana na kile alichokiita "mihimili ya Sunni na Shia".
-
Afrika Kusini: Tutafuta zaidi ya viza 2,000 zilizotolewa kupitia mitandao ya rushwa
Feb 24, 2026 07:41Afrika Kusini inajiandaa kufuta zaidi ya viza 2,000 ambazo zimepatikana kwa njia isiyo sahihi, huku serikali ikiendesha msako mkali wa kupambana na rushwa ndani ya Wizara ya Mambo ya Ndani.
-
Kwa nini Somaliland imeipa ofa Marekani ya kuanzisha kituo cha kijeshi katika ardhi yake?
Feb 24, 2026 05:09Somaliland imeipa Marekani ofa na fursa ya kuanzisha kambi ya kijeshi katika ardhi yake. Vyanzo vya habari vimeripoti kwamba, maafisa wa Somaliland wameipa Washington ofa ya kutumia rasilimali za madini za eneo hilo na kuanzisha kambi ya kijeshi.
-
Iran yaiambia Marekani: Vikwazo na vita vimefeli; jaribu diplomasia na kuheshimiana
Feb 24, 2026 04:32Mwanadiplomasia wa ngazi ya juu wa Iran amesema kuwa wakati umefika kwa Marekani kuachana na vikwazo vyake "visivyo na matunda" na sera iliyofeli ya vita dhidi ya Iran, akitilia mkazo kuheshimiwa kikamilifu diplomasia kama njia pekee ya kupiga hatua.
-
Venezuela yaitaka UN iishinikize Marekani imwachie huru Maduro wiki kadhaa baada ya kumteka nyara
Feb 24, 2026 04:32Venezuela imewasilisha ombi rasmi kwa Umoja wa Mataifa ikitaka kuachiwa huru mara moja Rais wa nchi hiyo Nicolas Maduro, kufuatia kutekwa nyara na wanajeshi wa Marekani katika operesheni ya mapema mwezi Januari mwaka huu ambayo Caracas imeitaja kuwa 'kinyume cha sheria'.
-
Afrika Kusini yatoa wito kwa nchi wanachama wa UN kulitambua taifa la Palestina
Feb 24, 2026 04:31Afrika Kusini jana Jumatatu ilitoa wito kwa nchi zote wanachama wa Umoja wa Mataifa kulitambua taifa la Palestina na kudhihirisha mshikamano na wananchi wa Palestina.
-
Sudan: Pendekezo lolote la kumaliza vita linapasa kulinda maslahi ya taifa na umoja wa ardhi ya nchi hiyo
Feb 24, 2026 04:30Sudan imesema kuwa pendekezo lolote la kumaliza vita na wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) linapasa kuzingatia maslahi makuu ya nchi hiyo, mshikamano na umoja wa ardhi nzima ya nchi hiyo.