-
Wanamgambo wanaoiunga mkono serikali: Tumewauwa wapiganaji 50 wa M23 mashariki mwa Kongo
Feb 24, 2026 04:29Wanamgambo wanaoiunga mkono serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamedai kuwa wamewauwa wapiganaji 50 waliokuwa wanachama wa kundi la waasi wa M23 na kuwateka nyara kadhaa katika mapigano makali hivi karibuni.
-
Machungu ya Ukoloni | Eritrea: Chini ya kivuli cha apathaidi ya Italia, simulizi ya udhalilishaji na mapambano
Feb 24, 2026 00:37Ukandamizaji wa kikoloni wa Italia nchini Eritrea haukuwa tu mradi wa upanuzi wa ushawishi wa kisiasa, bali ulikuwa mfumo uliosimikwa juu ya uvamizi wa kijeshi, ubaguzi wa rangi au apathaidi, ukandamizaji wa upinzani, na utumwa. Mfumo huu wa kikoloni ulifikia kilele mwaka 1938, katikati ya jiji la Roma, hatua ya malalmiko iliyochukuliwa na Zerai Deres ilipofichua wazi unafiki na ukatili wa utawala huo.
-
Pezeshkian: Iran inafuatilia diplomasia ya faida za pande zote katika uhusiano wake na Afrika
Feb 24, 2026 00:37Rais Masoud Pezeshkian amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaendelea kwa dhati kupanua ushirikiano wa kina na nchi za Afrika, kwa mujibu wa sera yake ya “diplomasia yenye mlingano” na msisitizo wa maslahi ya pamoja.
-
Wapalestina wanakoseshwa kufunga na kufungua Saumu kwa wakati kwenye jela za Israel
Feb 24, 2026 00:36Tume moja ya Palestina inayoshughulikia masuala ya Wapalestina wanaoshikiliwa kwenye jela za utawala wa kizayuni wa Israel imezishutumu mamlaka za jela hizo kwa kuwafanya Wapalestina hao washindwe kufunga Saumu zao "kwa wakati sahihi" katika mfungo huu wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
'Hapana, asante': Jibu la Waziri Mkuu wa Greenland kwa Trump kuhusu kuwapatia meli ya hospitali
Feb 24, 2026 00:36Waziri Mkuu wa Greenland Jens-Frederik Nielsen ameikataa ofa ya Rais wa Marekani Donald Trump ya kutuma meli ya hospitali katika eneo hilo la Denmark linalojiendeshea mambo yake, ambalo Trump amekuwa akilifuatilia kwa muda mrefu ili kulinyakua.
-
Chad yatangaza kufunga mpaka wake na Sudan kuzuia kuenea mapigano mpakani mwake
Feb 24, 2026 00:35Chad imetangaza kuwa, ili kuzuia kuenea mapigano kwenye maeneo ya mpakani, inaufunga mpaka wake wa pamoja na Sudan hadi itakapotolewa taarifa nyingine.
-
Waziri wa Ulinzi: Uhusiano na nchi za Afrika za kimapinduzi na zenye misimamo huru utastawishwa
Feb 23, 2026 23:01Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitizia kutekelezwa sera ya msingi ya kuendeleza na kustawisha uhusiano na nchi zenye misimamo huru na za kimapinduzi katika bara la Afrika Magharibi, hususan Burkina Faso.
-
Kutokubali Iran kusalimu amri mbele ya Marekani
Feb 23, 2026 22:51Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, akijibu mshangao wa Rais wa Marekani kuhusu sababu za Iran kutokubali kusalimu amri, aliandika kwa uwazi: “Hatusalimu amri kwa sababu sisi ni Wairani.”
-
'Kichapo ni hakika kwa adui': Kamanda Mkuu wa Jeshi la Iran abeza madai ya adui ya kutoshindwa
Feb 23, 2026 07:07Kamanda Mkuu wa Jeshi la Iran amebeza madai yanayotolewa na maadui ya kutoshindwa na kusema kuwa maadui hawakutarajia kuiona nchi hii ikionyesha umadhubuti wake mbele ya kuendelea kukusanya majeshi katika kanda hii.
-
Somalia yalaani shambulio la mauaji katika jimbo la Zamfara, Nigeria
Feb 23, 2026 07:06Somalia leo imelaani vikali shambulio la umwagaji damu katika jimbo la Zamfara kaskazini magharibi mwa Nigeria lililouwa raia wasiopungua 50. Wanawake na watoto pia walitekwa nyara katika hujuma hiyo ya kigaidi.