-
Maonyesho ya "Kisiwa cha Dhambi" yafanyika Magharibi mwa Kabul
May 22, 2026 04:09Maonyesho maalumu ya yanayodhihirisha uhalifu wa nchi za kibeberu pamoja na kashfa za kingono za viongozi wa nchi za Magharibi yaliyopewa jina "Kisiwa cha Dhambi" yanafanyika magharibi mwa mji mkuu wa Afghanistan, Kabul.
-
Ndoto ya Afrika isiyo na mpaka yakaribia baada ya Togo kuruhusu Waafrika kuingia nchini humo bila visa
May 22, 2026 03:58Togo imetangaza ruhusa kwa raia wa nchi zote za Afrika kuingia nchini humo bila visa na kukaa huko kwa hadi siku 30, mradi tu wawasilishe maombi kielektroniki kupitia jukwaa la serikali, saa 24 kabla ya kuwasili nchini Togo.
-
Wanaharakati 87 waliotekwa na vikosi vya Israel waanzisha mgomo wa njaa
May 21, 2026 13:37Angalau wanaharakati 87 waliotekwa nyara na vikosi vya Israel wakati wa uvamizi dhidi ya msafara wa misaada ya kibinadamu kuelekea Gaza, wameanzisha mgomo wa njaa, waandaaji wa safari hiyo walitangaza Jumatano.
-
Ujumbe wa safari ya Rais Putin nchini China kwa ulimwengu
May 21, 2026 13:34Siku nne tu baada ya kufanyika safari ya Rais Donald Trump wa Marekani nchini China, Rais Xi Jinping wa nchi hiyo amemkaribisha kwa shangwe Rais Vladimir Putin wa Russia mjini Beijing.
-
“Tutawafanya maadui wajute”: Qalibaf aonya dhidi ya njama za Marekani kuanzisha vita vipya
May 21, 2026 13:24Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, ametoa onyo kali akisema kuwa mienendo ya wazi na ya siri ya adui inaashiria wazi kuwa wanapanga kuanzisha duru nyingine ya vita.
-
Iran: UNSC Iivunje ukimya kuhusu vitisho vya Marekani na uhalifu wa kivita
May 21, 2026 13:05Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amelitaka Baraza la Usalama livunje ukimya wake kuhusu vitisho vya Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu na ukiukaji wa kimfumo wa sheria za kimataifa za kibinadamu uliofanyika wakati wa vita haramu vya hivi karibuni.
-
Jumuiya ya Nchi za Kiarabu yakemea mpango wa ‘Somaliland’ kufungua ubalozi katika al-Quds inayokaliwa kwa mabavu
May 21, 2026 13:00Jumuiya ya Nchi za Kiarabu (Arab League) imekosoa vikali uamuzi wa eneo la Somaliland lililojitenga na Somalia wa kufungua ubalozi katika mji mtakatifu wa al Quds (Jerusalem) unaokaliwa kwa mabavu na utawala wa Israel, ikisema hatua hiyo “haikubaliki kabisa.”
-
Ebola imeua watu 139, wengine 600 wameambukizwa DRC na Uganda
May 21, 2026 12:56Takriban wagonjwa 600 sasa wanashukiwa kuwa na Ebola na vifo 139 vikishukiwa kusababishwa na ugonjwa huo hali inayoongeza hofu ya kuenea zaidi kwa mlipuko wa sasa wa Ebola.
-
Kiongozi Muadhamu amkumbuka Shahidi Rais Raeisi, ampongeza kwa uwajibikaji
May 21, 2026 04:42Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, ametoa ujumbe wa kuadhimisha mwaka wa pili tangu kufa shahidi aliyekuwa Rais wa zamani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Sayyid Ebrahim Raeisi. Katika ujumbe huo, alimwelezea marehemu Rais Raeisi kama kiongozi aliyekuwa na hisia ya juu ya uwajibikaji, mwenye kuzingatia uadilifu, mwenye kuendesha diplomasia hai na yenye manufaa, na hasa aliyekuwa karibu na wananchi kwa unyenyekevu na huruma.
-
IRGC yaonya kuwa vita vipya dhidi ya Iran vitavuka mipaka ya eneo
May 21, 2026 04:40Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetoa onyo kali kwamba endapo vita dhidi ya Iran vitaanzishwa tena, basi vita vya kikanda vilivyoahidiwa hapo awali safari hii vitapanuka kuvuka eneo la Asia Magharibi, na kwamba mapigo mazito yataelekezwa kutoka maeneo ambayo adui hawezi kuyadhania.