-
Iran yakosoa upotoshaji wa CENTICOM kuhusu mauaji ya halaiki ya Minab
May 21, 2026 04:36Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amekadhibisha matamshi ya Kamandi Kuu ya Marekani (CENTCOM) kuhusu mashambulizi ya ya makombora yaliyofanywa katika shule ya msingi ya Shajareh Tayyebeh huko Minab kusini mwa Iran na kuyataja kuwa "yasiyo na msingi".
-
UNICEF: Mlipuko wa Ebola umewaweka Watoto hatarini
May 21, 2026 04:33Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, limesema lina wasiwasi mkubwa kuhusu mlipuko wa Ebola unaoendelea katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC na Uganda, huku likionya kuwa watoto wako kwenye hatari kubwa zaidi.
-
Putin na Xi walaani vita vya uchokozi vya Marekani na Israel dhidi ya Iran
May 21, 2026 04:28Rais wa Russia, Vladimir Putin, na mwenzake wa Jamhuri ya Watu wa China, Xi Jinping, wamekemea kwa pamoja vita vya hivi karibuni vya uchokozi vilivyoanzishwa na Marekani na Israel dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, wakisisitiza kwamba njia pekee ya kumaliza mzozo huo unaotishia uthabiti wa kanda ni kupitia mazungumzo na diplomasia.
-
Kiongozi Muadhamu: Nguvu inayojitokeza ya Iran inahusiana moja kwa moja na ongezeko la idadi ya watu
May 20, 2026 11:12Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei amesema kupanda hadhi ya Iran ya kuwa taifa kubwa na lenye taathira kunahusiana moja kwa moja na ongezeko la idadi ya watu wake, na kutoa wito wa kuzidishwa juhudi za kukuza utamaduni wa kuzaa watoto.
-
Mkuu wa vyombo vya mahakama: Shahidi Raisi alijitolea kuwatumikia wananchi
May 20, 2026 11:09Mkuu wa vyombo vya Mahakama vya Iran anasema kuwa Rais Shahidi Ebrahim Raisi alijitolea kwa dhati kuwatumikia wananchi na kusabilia maisha yake kwa ajili ya Iran.
-
Iran yatahadharisha kuhusu Marekani kulitumia vibaya Baraza la Usalama la UN
May 20, 2026 11:06Mwakilishi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa ameeleza kuwa: "Marekani inalitumia vibaya Baraza la Usalama kwa kueneza uwongo na tuhuma zisizo na msingi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na mpango wake wa nyuklia."
-
Viongozi wa China na Russia: Tunafanya kazi ili kuasisi utaratibu wa kiadilifu na haki zaidi duniani
May 20, 2026 11:04Viongozi wa China na Russia wamesisitiza mwanzoni mwa mazungumzo yao kuhusu azimio la pamoja la nchi hizo mbili la kuasisi utaratibu wa haki zaidi wa kimataifa na ulimwengu wa kambi kadhaa.
-
Rwanda yaimarisha udhibiti wa mpakani kutokana na mlipuko hatari wa Ebola nchini Kongo
May 20, 2026 10:58Mamlaka ya Rwanda imeongeza hatua za uchunguzi wa afya na kuimarisha udhibiti katika mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo huku mlipuko hatari wa homa ya Ebola ukiendelea kuitatiza Kongo.
-
Arsenal yatwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza baada ya Man City kulazimishwa sare na FC Bournemouth
May 20, 2026 03:56Hatimaye baada ya miaka 22 ya ukame, Arsenal au ukipenda waite The Gunners wametwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) msimu wa 2025-26 baada ya Man City kulazimishwa sare ya bao moja kwa moja na The Cherries ambao nao walikuwa wanafukuzia angalau alama moja ili wafaulu kushiriki kombe la Uefa Conference Cup msimu ujao.
-
Jeshi la Iran: Medani mpya za mapambano zitafunguliwa ikiwa adui atatumbukia katika mtego wa Israel
May 20, 2026 03:26Jeshi la Iran limeonya kuwa iwapo adui ataanguka tena katika mtego wa Israel na kuanzisha uchokozi mwingine dhidi ya Iran, jeshi la taifa litafungua medani mpya ya mapambano kwa kutumia zana na mbinu mpya.