-
Kutokubali Iran kusalimu amri mbele ya Marekani
Feb 23, 2026 22:51Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, akijibu mshangao wa Rais wa Marekani kuhusu sababu za Iran kutokubali kusalimu amri, aliandika kwa uwazi: “Hatusalimu amri kwa sababu sisi ni Wairani.”
-
'Kichapo ni hakika kwa adui': Kamanda Mkuu wa Jeshi la Iran abeza madai ya adui ya kutoshindwa
Feb 23, 2026 07:07Kamanda Mkuu wa Jeshi la Iran amebeza madai yanayotolewa na maadui ya kutoshindwa na kusema kuwa maadui hawakutarajia kuiona nchi hii ikionyesha umadhubuti wake mbele ya kuendelea kukusanya majeshi katika kanda hii.
-
Somalia yalaani shambulio la mauaji katika jimbo la Zamfara, Nigeria
Feb 23, 2026 07:06Somalia leo imelaani vikali shambulio la umwagaji damu katika jimbo la Zamfara kaskazini magharibi mwa Nigeria lililouwa raia wasiopungua 50. Wanawake na watoto pia walitekwa nyara katika hujuma hiyo ya kigaidi.
-
Kiongozi wa chama cha BSW Ujerumani atoa wito kwa nchi yake kuondoa vikwazo dhidi ya Iran
Feb 23, 2026 06:31Kiongozi wa chama cha Union for Reason and Justice cha Ujerumani, Sarah Wagenknecht, anatoa wito kwa serikali ya nchi yake kuondoa vikwazo vilivyowekwa dhidi ya Iran na kuzuia Marekani kutumia kambi za kijeshi nchini Ujerumani kuanzisha mashambulizi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Mafuriko mashariki mwa Kongo yameacha zaidi ya kaya 2,500 bila makazi
Feb 23, 2026 06:30Zaidi ya kaya 2,500 zimeachwa bila makazi baada ya mito miwili kuvunja kingo zake na kusababisha mafuriko katika vijiji kadhaa katika eneo la kati, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Mwandishi wa habari mtajika wa Marekani: Israel ni mzigo mkubwa zaidi wa kigeni kwa Marekani
Feb 23, 2026 06:05Mwandishi mashuhuri wa habari wa Marekani, amekosoa waziwazi sera za Washington kuhusu Israel, akisema utawala huo ni mzigo mkubwa zaidi wa kigeni kwa Marekani.
-
Spoti, Feb 23
Feb 23, 2026 04:43Huu ni mkusanyiko wa baadhi ya matukio muhimu ya michezo yaliyoshuhudiwa ndani ya siku saba zilizopita kitaifa, kieneo na kimataifa.
-
Pezeshkian: Kuna ishara 'ya kutia moyo' katika mazungumzo na Marekani, lakini Iran iko tayari kwa hali yoyote
Feb 23, 2026 03:39Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, amekaribisha ishara ya "kutia moyo" katika mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja na Marekani kuhusu mpango wa nyuklia wa amani wa Tehran lakini amesema Jamhuri ya Kiislamu iko tayari kwa "hali yoyote inayowezekana."
-
Mkutano wa dharura wa mawaziri wa mambo ya nje wa OIC kujadili unyakuzi wa Israel wa ardhi za Palestina
Feb 23, 2026 03:39Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) itafanya mkutano wa dharura katika ngazi ya mawaziri wa mambo ya nje Alhamisi ijayo kujadili maamuzi ya hivi karibuni ya Israel yanayozidisha ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni na unyakuzi wa ardhi za Palestina katika Ukingo wa Magharibi.
-
Velayati: Kashfa ya Epstein ilikuwa mwisho wa ustaarabu wa Magharibi
Feb 23, 2026 03:38Mshauri wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu kuhusu masuala ya kimataifa amesema: "Uchunguzi kuhusu kesi ya wanasiasa wa Marekani na washirika wao wa Magharibi katika kadhia ya Jeffrey Epstein umeibua kashfa kubwa katika nchi za Magharibi katika nyanja zote."