-
Amnesty International: Serikali ya Marekani inakandamiza vyombo vya habari na kuvizuia kueleza ukweli
Jan 31, 2026 03:40Shirika la Msamaha Duniani la Amnesty International limetangaza kuwa, serikali ya Marekani inakandamiza vyombo vya habari na kuvizuia kueleza ukweli.
-
OCHA: Watu milioni moja Gaza wanahitaji makazi na msaada wa haraka
Jan 31, 2026 03:34Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Uratibu wa Misaada ya Kibinadamu (OCHA) imeonya kwamba, hali ya kibinadamu huko Gaza bado ni mbaya, huku zaidi ya watu milioni moja wakihitaji makazi na msaada wa haraka.
-
Ushirikiano wa Starmer na Trump; madai mapya dhidi ya mpango wa nyuklia wa amani wa Iran
Jan 31, 2026 00:04Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer ametoa tuhuma zisizo na msingi dhidi ya mpango wa nyuklia wa amani wa Iran.
-
Mgogoro mkali wa kidiplomasia.. Afrika Kusini na Israel zawatimua wanadiplomasia
Jan 31, 2026 00:01Uhusiano wa kidiplomasia kati ya Israel na Afrika Kusini uliingia katika mgogoro mkubwa na usio wa kawaida jana Ijumaa, baada ya pande zote mbili kutangaza maafisa wa kidiplomasia wa kila upande kuwa watu wasiofaa na kuwaamuru waondoke ndani ya saa 72.
-
Pezeshkian amweleza Erdogan: Iran inapinga vitisho, inaunga mkono mazungumzo na diplomasia
Jan 30, 2026 23:27Iran inapinga vitisho na kushurutishwa na ina azma thabiti ya kufanya mazungumzo, kuheshimiana pande mbili na kutekelezwa diplomasia kwa manufaa ya pande zote. Haya yameelezwa na Rais Masoud Pezeshkian huku Washington ikiendelea kutoa vitisho vya kijeshi dhidi ya Tehran.
-
Mkuu wa AU aeleza wasiwasi wake kuhusu kuongezeka mivutano katika eneo la Tigray, Ethiopia
Jan 30, 2026 23:23Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika jana Ijumaa alitoa wito kwa pande zinazozozana kujiepusha na mivutano haraka iwezekanavyo baada ya vyombo vya habari kuripoti kwamba safari za ndege zimesimamishwa katika eneo la Tigray kaskazini mwa Ethiopia kutokana na mapigano ya silaha yaliyoibuka katika eneo hilo.
-
Araqchi: Iran iko tayari kwa vita na mazungumzo
Jan 30, 2026 23:16Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi, amesema kuwa Tehran iko tayari kwa vita na mazungumzo lakini haitakubali kuwekewa masharti. Araqchi ameeleza haya kufuatia vitisho vya kijeshi vya Washington dhidi ya Tehran.
-
UNICEF: Mgogoro mkubwa zaidi duniani: Sudan ina wakimbizi wa ndani milioni 9.5
Jan 30, 2026 23:12Mfuko wa Kuhudumia Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) amesema kuwa Sudan imekumbwa na mgogoro mkubwa zaidi wa wakimbizi wa ndani duniani, huku takriban watu milioni 9.5 wakilazimika kuhaka makazi yao katika majimbo 18.
-
Khatibu wa Swala ya Ijumaa Tehran: Marekani haiwezi kukariri upumbavu wa huko nyuma
Jan 30, 2026 09:12Khatibu wa Swala ya Ijumaa iliyoswaliwa leo hapa mjini Tehran amesema: "Vita vya siku 12 viliiweka Iran katika nafasi maalum na ya kipekee ya nguvu, na nina uhakika kwamba Marekani haiwezi kukariri upumbavu wa huko nyuma.
-
Kucheza na moto kwa Trump kunaweza kusababisha mzozo kamili kanda ya Asia Magharibi
Jan 30, 2026 08:30Iran imetangaza kwamba kauli za "kuchochea vita" za Donald Trump zinazidisha mvutano wa kikanda.