-
Kuongezeka tofauti katika safu ya uongozi nchini Marekani kuhusiana na suala la Afghanistan
Mar 30, 2017 22:02Katika hali ambayo makamanda wa jeshi la Marekani hususan John Joseph Nicholson, kamanda wa jeshi la nchi hiyo na Muungano wa Kijeshi wa Nchi za Magharibi (NATO) nchini Afghanistan wanasisitiza udharura wa kuongezwa askari nchini humo, vyombo mbalimbali vya habari nchini Marekani vimeripoti kwamba baadhi ya wabunge wa nchi hiyo wanafanya juhudi za kutaka kuhitimishwa uwepo wa askari wa nchi hiyo huko Afghanistan.
-
Daesh laua zaidi ya watu 30 katika hospitali ya kijeshi Afghanistan
Mar 08, 2017 12:33Wanamgambo waliojizatiti kwa silaha nzito wameua zaidi ya watu 30 na kuwajeruhi wengine wapatao 50 katika shambulio walilofanya dhidi ya hospitali kubwa zaidi ya kijeshi ya Sardar Daud Khan iliyopo katikati mwa mji mkuu wa Afghanistan, Kabul.
-
Rais Ashraf Ghani: Lengo la makundi 20 ya kigaidi ni kuisambaratisha nchi
Feb 27, 2017 23:14Rais Ashraf Ghani wa Afghanistan amesema kuwa makundi 20 ya kigaidi ambayo yanaendesha harakati zao katika maeneo tofauti ya nchi hiyo dhidi ya raia na askari wa usalama, yana lengo la kulisambaratisha taifa hilo.
-
Afghanistan: Mamia ya wanawake wanafanywa watumwa wa ngono na kundi la ISIS nchini mwetu
Feb 20, 2017 04:40Mkuu wa Taasisi ya 'Uadilifu kwa ajili ya Wote' nchini Afghanistan amesema kuwa, kundi la kigaidi na ukufurishaji la Daesh limewafanya watumwa wa ngono zaidi ya wanawake 100 katika miji tofauti ya mkoa wa Nangarhar nchini humo ndani ya kipindi cha miaka miwili iliyopita.
-
UN: 2016 ulikuwa mwaka wa maafa makubwa zaidi kwa raia wa Afghanistan
Feb 06, 2017 11:31Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Msaada kwa Afghanistan (UNAMA) umetangaza kuwa jumla ya raia 3,498 waliuliwa na wengine 7,920 walijeruhiwa katika mwaka 2016 nchini Afghanistan, maafa ambayo kwa sehemu moja yamechangiwa na ongezeko la mashambulio ya kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh na mashambulio ya anga ya madola ya kigeni.
-
100 waaga dunia kutokana na maporomoko ya theluji Afghanistan, Pakistan
Feb 06, 2017 04:15Makumi ya watu wamepoteza maisha kutokana na maporomoko ya theluji katika nchi za Afghanistan na Pakistan.
-
Trump: Marekani ilifanya makosa kuzivamia nchi za Iraq na Afghanistan
Jan 16, 2017 03:03Rais mteule wa Marekani amesema kuwa nchi hiyo ilifanya makosa kuzivamia nchi za Iraq na Afghanistan.
-
Vikosi vya jeshi la Marekani vyakiri kuua raia 33 wa Afghanistan
Jan 12, 2017 11:58Vikosi vya jeshi la Marekani vilivyoko chini ya mwavuli wa shirika la kijeshi la NATO vimekiri kuwa viliua raia 33 wa Afghanistan wakiwemo watoto wadogo katika shambulio la mwezi Novemba jana lililofanywa kwa kisingizio cha kupambana na wanamgambo wa kundi la Taliban.
-
Magaidi washambulia msikiti kwa bomu na kuua makumi Kabul, Afghanistan
Nov 22, 2016 02:51Makumi ya watu wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa katika shambulizi la kigaidi lililolenga msikiti wa Kishia katika mji mkuu wa Afghanistan, Kabul, wakati wa maadhimisho ya Arubaini ya Imam Hussein AS.
-
Marekani yatuhumiwa na ICC kutenda jinai za kivita Afghanistan
Nov 15, 2016 23:26Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC ametoa taarifa akiituhumu Marekani kwamba, imetenda jinai za kivita nchini Afghanistan.