-
Iran: Afrika isigeuzwe kimbilio la magenge ya kigaidi na ukufurishaji
Nov 24, 2017 12:25Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitizia udharura wa kufanyika jitihada za kuzuia bara la Afrika kugeuka kuwa kimbilio na kitovu cha magenge ya kigaidi na yenye misimamo ya kufurutu ada, kufuatia kusambaratishwa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh (ISIS) katika nchi za Syria na Iraq.
-
Waislamu Mombasa Kenya walalamikia mavazi ya nusu uchi + Sauti
Nov 24, 2017 02:41Waislamu nchini Kenya wamekosoa vikali tabia ya baadhi ya vijana kuvaa mavazi yasiyo ya heshima na kutoa mwito kwa serikali ya Kenya kuiga mfano wa Uganda ambayo inashinikiza mavazi ya heshima hasa katika maeneo ya umma. Seifullah Murtadha na maelezo zaidi
-
Rwanda kupokea maelfu ya wahamiaji waliokwama Libya + Sauti
Nov 24, 2017 02:36Serikali ya Rwanda imesema kuwa iko tayari kupokea wahamiaji zaidi ya 30,000 wa Kiafrika waliokwama nchini Libya na ambao wanapigwa mnada sokoni na kuuzwa kama bidhaa.
-
Interpol yawatia nguvuni watu 40 kwa kufanya magendo ya binadamu Libya
Nov 24, 2017 01:03Watu wasiopungua 40 wametiwa mbaroni kwa tuhuma za kufanya magendo ya binadamu katika eneo la magharibi mwa Afrika baada ya kusambaa mkanda wa video unaoonesha wakimbizi wa Kiafrika wakipigwa mnada na kuuzwa kama bidhaa nchini Libya.
-
Wakuu wa Ulinzi Afrika Mashariki wakutana Uganda
Nov 20, 2017 23:10Wataalamu wa masuala ya ulinzi kutoka nchi za Afrika Mashariki wanakutana nchini Uganda kujadili njia za kuimarisha amani na usalama kieneo.
-
Hali mbaya ya wahajiri wa Afrika nchini Libya
Nov 20, 2017 07:53Sambamba na kuendelea hali mbaya ya wakimbizi na wahajiri wa Kiafrika nchini Libya, Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa ameutuhumu Umoja wa Ulaya kwamba, unapuuza hali mbaya wanayokabiliwa nayo wahajiri wa Kiafrika.
-
AU yasema Libya imegeuzwa kuwa kitovu cha soko la utumwa duniani
Nov 18, 2017 03:59Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika AU ametoa mwito kwa vyombo vya dola nchini Libya kuanzisha uchunguzi juu ya ripoti zinazosema kuwa nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika ni kitovu cha biashara ya utumwa.
-
Sisitizo la Senegal juu ya kudhaminiwa usalama katika nchi za bara la Afrika
Nov 14, 2017 08:33Katika kikao cha nne cha Kongamano la Amani na Usalama wa Afrika Rais Macky Sall wa Senegal amesisitizia ulazima wa kutolewa misaada kwa ajili ya kudhaminiwa usalama wa nchi za bara hilo.
-
Watu 7 wauawa na 20 wajeruhiwa Jamhburi ya Afrika ya Kati
Nov 13, 2017 11:52Habari kutoka Bangui, mji mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) zinasema kuwa watu saba wameuawa na wengine 20 kujeruhiwa baada ya kutokea shambulizi la guruneti katika eneo la starehe na katika machafuko ya ulipizaji kisasi siku mbili mfululizo mjini humo.
-
Ombi la kutaka Afrika itengewe viti viwili vya kudumu katika Baraza la Usalama
Nov 12, 2017 09:45Mwakilishi wa Algeria katika Umoja wa Mataifa, ametoa mwito wa kufanyika marekebisho katika muundo wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kutengewa Afrika viti viwili vya kudumu kkatika baraza hilo.