-
Waalgeria waandamana hadi hospitali alikolazwa Bouteflika nchini Uswisi
Mar 09, 2019 00:52Waalgeria wanaoishi nchini Uswisi wamefanya maandamano ya kupinga msimamo wa Rais Abdelaziz Bouteflika wa kugombea tena urais kwa muhula wa tano.
-
Rais Bouteflika azidi kubanwa; awaonya wafanya maandamano dhidi yake
Mar 08, 2019 12:01Rais Abdelaziz Bouteflika wa Algeria ametoa onyo lake la kwanza kwa maelfu ya raia wanaoandamana katika mitaa mbalimbali ya nchi hiyo wakitaka ahitimishe utawala wake wa miaka 20. Amesema kuwa ghasia na machafuko yatayumbisha nchi.
-
Nchi za Magharibi zavunja kimya, zaitaka Algeria iheshimu haki za raia
Mar 06, 2019 04:46Nchi za Magharibi zimevunja kimya chao cha muda sasa mbele ya ukandamizaji mkubwa unaofanywa na vyombo vya dola nchini Algeria dhidi ya raia wanaopinga uamuzi wa rais mgonjwa wa nchi hiyo wa kutaka kugombea tena kiti hicho na kuitaka serikali ya Algiers iheshimu haki za raia ikiwemo haki ya kufanya maandamano ya amani.
-
Maandamano yashika kasi Algeria, jeshi laapa kuzuia umwagikaji damu
Mar 05, 2019 23:23Maelfu ya wananchi wa Algeria Jumanne waliendeleza maandamano katika mji mkuu Algiers, wakimtaka Rais Abdelaziz Bouteflika aondoke madarakani huku jeshi nalo likiapa kuzuia umwagikaji damu nchini humo.
-
Wanafunzi Algeria wagoma kuingia madarasani kupinga msimamo mpya wa Bouteflika
Mar 05, 2019 04:31Wanafunzi wa vyuo vikuu nchini Algeria ambao wameonyesha kuwa na dhamira ya kuongoza maandamano makubwa zaidi dhidi ya serikali kuwahi kushuhudiwa nchini humo kwa miaka kadhaa sasa, jana waligoma kuingia madarasani ili kuonyesha upinzani wao kwa pendekezo la Rais Abdelaziz Bouteflika la kugombea tena urais katika uchaguzi utakaofanyika mwezi ujao, lakini kutobaki madarakani kwa muhula wote endapo atachaguliwa tena.
-
Rais wa Algeria asisitiza kugomeba urais huku maandamano dhidi yake yakishadidi
Mar 04, 2019 23:14Hatimaye muhula wa mwisho wa kujiandikisha kisheria kugombea urais wa Algeria ulipowadia, Rais Abdelaziz Bouteflika, alijiandikisha rasmi kugombea tena katika uchaguzi huo. Katika barua yake kwa watu wa Algeria, ameahidi kuwa akichaguliwa atahakikisha kuna katiba mpya ambayo itapigiwa kura ya maoni na wananchi ili kuwepo mfumo mpya wa utawala nchini humo.
-
Rais wa Algeria aahidi kung'atuka madarakani ndani ya mwaka mmoja endapo atachaguliwa tena
Mar 03, 2019 23:55Rais Abdelaziz Bouteflika wa Algeria anayekabiliwa na upinzani wa umma baada ya kuweko madarakani kwa muda wa miaka 20, amesema atagombea tena urais kwa mara ya tano katika uchaguzi uliopangwa kufanyika mwezi Aprili, lakini ameahidi kung'atuka madarakani na kuitisha uchaguzi wa mapema ndani ya muda wa mwaka mmoja endapo atachaguliwa tena.
-
Chama cha Wafanyakazi kususia uchaguzi wa urais Algeria
Mar 03, 2019 04:29Chama cha Wafanyakazi nchini Algeria kimetangaza kuwa hakitashiriki katika uchaguzi wa urais unaotazamiwa kufanyika Aprili 18 mwaka huu.
-
Makumi ya maelfu ya Waalgeria waandamana kutaka rais Bouteflika ang'atuke madarakani
Mar 02, 2019 12:47Makumi ya maelfu ya watu wameandamana katika miji mbalimbali nchini Algeria kutaka rais wa nchi hiyo Abdelaziz Bouteflika aondoke madarakani. Maandamano hayo ya jana Ijumaa ni makubwa zaidi kufanywa dhidi ya serikali tangu yale ya miaka minane nyuma wakati wa vuguvugu la Machipuo ya Kiarabu yaliyojulikana pia kama Mwamko wa Kiislamu.
-
Kushadidi ghasia na machafuko nchini Algeria
Mar 02, 2019 11:32Maandamano ya wananchi wa Algeria dhidi ya uamuzi wa Rais wa sasa wa nchi hiyo, Abdelaziz Bouteflika wa kutaka kugombea tena kiti cha urais katika uchaguzi ujao yameitumbukiza nchi hiyo katika mgogoro mkubwa wa kisiasa na hadi sasa watu wasiopungua 10 wameuliwa katika mapigano kati ya waandamanaji na polisi huko Algiers mji mkuu wa nchi hiyo.