Rais wa Syria amesema kuwa kuwepo mshikamamo baina ya nchi za Kiarabu na kutekeleza hatua za pamoja kutapelekea kupatikana amani na uthabiti katika eneo.
Kwa akali wakufunzi watano wa kijeshi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) na Bahrain wameuawa katika shambulizi linaloaminika kufanywa na wanachama wa kundi la kigaidi la al-Shabaab huko Mogadishu, mji mkuu wa Somalia.
Sheikh Issa Qassim Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Bahrain ameitaja hatua ya Manama ya kushiriki katika muungano wa baharini unaoongozwa na Marekani katika Bahari ya Sham dhidi ya Yemen kuwa ni kitendo kibaya, chenye kutia uchungu na cha fedheha.
Chama kikuu cha upinzani nchini Bahrain cha al-Wefaq kimesema hatua ya utawala wa Aal-Khalifa ya kujiunga na muungano wa baharini wa Marekani katika Bahari Nyekundu ni kusaliti kadhia ya Palestina.
Naibu Spika wa Bunge la Kitaifa la Bahrain amesema Wabunge wa nchi hiyo wanakishinikiza chombo hicho cha kutunga sheria kubatilisha uhusiano wa kawaida baina ya nchi hiyo ya Kiarabu ya Ghuba ya Uajemi na utawala wa Kizayuni wa Israel.
Bunge la Bahrain limetangaza kuwa, limesitisha uhusiano wa kiuchumi na utawaa wa Kizayuni wa Israel na kuwaondoa mabalozi wake kutokana na kuendelea mashambulio ya jeshi la Israel dhidi ya wakazi wa Ukanda wa Gaza.
Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya Lebanon imeujia juu utawala wa Aal-Khalifa wa Bahrain kwa kuuruhusu utawala haramu wa Israel kufungua ubalozi wake katika nchi hiyo ya Kiarabu ya Ghuba ya Uajemi.
Baadhi ya akina mama wa wafungwa wa kisiasa nchini Bahrain wameanza mgomo wa kususia kula wakipinga hali mbaya ya magereza na kuwaunga mkono watoto wao.
Wananchi wa Bahrain wamefanya maandamano katika miji mbalimbali ya nchi hiyo ukiwemo mji mjuu Manama, kwa shabaha ya kuwaunga mkono na kusimama pamoja na wafungwa waliogoma kula wakilalamikia hali mbaya ya jela.
Mrengo mkubwa zaidi wa upinzani Bahrain umekosoa vikali azma ya utawala wa Aal-Khalifa ya kuwaajiri madaktari wa utawala haramu wa Israel katika nchi hiyo ya Kiarabu.