-
Kukiri Jared Kushner kutofanikiwa mkutano wa Manama, kufeli hatua ya kwanza ya Muamala wa Karne
Jul 10, 2019 05:29Katika hatua za uungaji mkono wake wa kila upande kwa utawala haramu wa Kizayuni Israel, rais wa Marekani, Donald Trump amekuwa akifanya njama mbalimbali kufanikisha uadui wake dhidi ya taifa linalodhulumiwa la Palestina.
-
Kushner akiri: Mkutano wa kuzindua "Muamala wa Karne" Bahrain umefeli
Jul 08, 2019 06:06Jared Kushner, mkwe wa Rais Donald Trump wa Marekani amekiri kwamba, Waplestina wameufanya mkutano wa kiuchumi wa Bahrain, uliokuwa umeitishwa kuzindua mpango wa Mualama wa Karne dhidi ya taifa la Palestina, ushindwe na kufeli.
-
Hamas yaapa kudumaza mpango wa Trump wa "Muamala wa Karne"
Jul 06, 2019 21:54Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesema kuwa itaendeleza harakati za kupinga mpango eti wa amani uliozusha makelele mengi wa Rais Donald Trump wa Marekani baina ya utawala haramu wa Israel na Wapalestina uliopewa jina la "Muamala wa Karne"
-
Ansarullah: Mkutano wa Bahrain ni uhaini dhidi ya Wapalestina
Jun 28, 2019 10:31Kiongozi wa harakati ya Ansarullah ya Yemen amesema kuwa, mkutano wa Marekani uliofanyika siku chache zilizopita katika mji mkuu wa Bahrain, Manama kwa shabaha ya kuzindua Muamala wa Karne ni hujuma ya moja kwa moja na uhaini dhidi ya wananchi madhulumu wa Palestina.
-
Bahrain: Tunataka kuimarisha uhusiano wetu na Israel
Jun 27, 2019 21:59Bahrain ambayo ilikuwa mwenyeji wa eti mkutano wa kiuchumi wa mjini Manama baada ya kuficha kwa muda mrefu uhusiano wake na utawala wa Kizayuni wa Israel, hatimaye imefunguka na kusema kuwa inataka kuwa na amani na kuimarisha uhusiano wake na utawala huo haramu.
-
Sheikh Isa Qassim: Trump anataka kuiuza Palestina na matukufu yake
Jun 25, 2019 02:25Mwanazuoni maarufu wa Kiislamu nchini Bahrain, Sheikh Isa Qassim sambamba na kulaani hatua ya utawala wa Manama kuwa mwenyeji wa Kongamano la Kibiashara linalotazamiwa kuanza leo nchini humo kwa shabaha ya kuzindua mpango wa 'Muamala wa Karne' amesema mpango huo wa Rais Donald Trump wa Marekani unakusudia kuwapokonya Wapalestina haki zao zote na kuuza kila kitu kinachomilikiwa nao yakiwemo maeneo matakatifu.
-
Wamorocco waandamana kupinga mkutano wa Bahrain wa kuangamiza kadhia ya Palestina
Jun 24, 2019 02:03Maelfu ya wananchi wa Morocco wamefanya maandamano makubwa kupinga mkutano wa kufungua mpango wa Marekani wa Muamala wa Karne wa kuangamiza kadhia ya Palestina uliopangwa kufanyika kesho na keshokutwa Jumatano katika mji mkuu wa Bahrain, Manama.
-
Saeb Erekat: Siasa za Marekani katika mkutano wa Bahrain zitafeli
Jun 21, 2019 02:53Katibu wa Chama cha Ukombozi wa Palestina (PLO), Saeb Erekat amesema kuwa siasa za Marekani katika kikao cha uchumi kinachosimamiwa na Washington nchini Bahrain, zitashindwa tu.
-
Wafanyabiashara wa Kipalestina wasusia mkutano wa Trump, Bahrain
Jun 21, 2019 00:08Wafanyabiashara na wawekezaji mashuhuri wa Kipalestina wametangaza bayana kuwa hawatoshiriki mkutano wa 'kiuchumi wa Manama' nchini Bahrain ulioitishwa na Marekani, wenye lengo la kuzindua 'Muamala wa Karne', wakisisitiza kuwa kile ambacho Wapalestina wanahitajia ni uhuru wao na wala sio fedha.
-
Israel kushiriki mkutano wa Marekani dhidi ya Wapalestina, Bahrain
Jun 17, 2019 03:16Utawala wa Kizayuni wa Israel umethibitisha kuwa utashiriki mkutano wa 'kiuchumi wa Manama' nchini Bahrain ulioitishwa na Marekani, wenye lengo la kuzindua 'Muamala wa Karne'.