-
Umoja wa Mataifa watoa wito wa kusaidiwa wakimbizi Waislamu Warohingya
Mar 17, 2018 07:59Umoja wa Mataifa umetoa wito wa kukusanywa misaada kwa ajili ya kuwasaidia wakimbizi takribani milioni moja wa jamii ya Rohingya wa Myanmar ambao wako katika kambi za wakimbizi nchini Bangladesh sambamba na kuandaliwa mazingira ya Waislamu hao kurejea nchini kwao.
-
Makumi ya watu wapoteza maisha baada ya ndege kuanguka Kathmandu, Nepal
Mar 12, 2018 13:51Ndege ya abiria iliyokuwa imebaba watu 71 kutoka Bangladesh imeanguka wakati ikitua katika uwanja wa ndege wa Kathmandu, mji mkuu wa Nepal ambapo taarifa zainasema makumi ya watu wamefariki.
-
UN yasema mauaji dhidi ya Waislamu wa Rohingya yanaendelea Myanmar
Mar 06, 2018 07:58Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa imetahadharisha kuhusiana na kuendelea mauaji ya kizazi yanayofanywa na serikali ya Myanmar dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya magharibi mwa nchi hiyo.
-
Bangladesh yalalamikia hatua ya Myanmar kuweka askari wake wengi karibu na eneo walipo Waislamu
Mar 02, 2018 14:18Wizara ya Mambo ya Nje ya Bangladesh imelalamikia hatua ya Myanmar ya kuongeza idadi ya askari wake katika eneo lililo karibu na kambi za maelfu ya Waislamu wa Rohingya katika sehemu ya uzio wa mpaka baina ya nchi mbili.
-
Uamuzi wa Bangladesh wa "kuwatupa" Waislamu wa Rohingya katika visiwa visivyo na watu
Feb 23, 2018 16:58Serikali ya Bangladesh imetangaza kuwa, viongozi wa nchi hiyo wana nia ya kuwapeleka Waislamu wa jamii ya Rohingya katika visiwa visivyokaliwa na watu kwenye Ghuba ya Bengal.
-
Kuwasilishwa kwa Myanmar orodha ya kwanza ya Waislamu wa Rohingya watakaorejeshwa nchini humo
Feb 18, 2018 08:13Waziri wa Mambo ya Ndani wa Bangladesh ameikabidhi Myanmar orodha ya kwanza ya wakimbizi wa Waislamu wa kabila la Rohingya ambao wanatazamiwa kurejeshwa katika makazi yao.
-
UNICEF yataka kuandaliwa mazingira ya kurejea wakimbizi watoto wa Myanmar
Jan 25, 2018 07:24Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa umetoa wito wa kuboreshwa mazingira ya kiusalama na kuandaliwa uwanja wa kurejea nchini Myanmar wakimbizi watoto wa Kiislamu wa jamii ya Rohingya walioko nchini Bangladesh.
-
Warohingya walioko Bangladesh wakataa kurejeshwa nchini Myanmar
Jan 19, 2018 13:53Mamia ya wakimbizi wa Kirohingya walioko nchini Bangladesh leo Ijumaa wamefanya maandamano wakipinga mpango wa kuwarejesha nchini Myanmar, ambako walikimbia mauaji na mashambulizi kutoka kwa jeshi la nchi hiyo likishirikiana na Mabudha wenye misimamo mikali.
-
EU: Idadi ya watoto mayatima wa Rohingya waliokimbilia Bangladesh ni 40,000
Nov 02, 2017 07:31Kamishna Mkuu wa Misaada ya Kibinadamu na Kudhibiti Majanga wa Umoja wa Ulaya amesema zaidi ya watoto elfu 40 ni miongoni mwa malaki ya wakimbizi wa jamii ya Rohingya waliokimilia nchini Bangladesh kutokana na mauaji na ukandamizaji unaofanywa dhidi yao na serikali ya Myanmar.
-
Bangladesh kufunga uzazi wakimbizi Waislamu Warohingya kutoka Myanmar
Oct 28, 2017 15:37Maafisa wa afya nchini Bangladesh wamesema wameanzisha mpango maalumu wa kupunguza idadi ya wakimbizi Waislamu wa jamii ya Rohingya ambao wamekimbia mauaji ya kimbari huko Myanmar na kujazana katika kambi za wakimbizi nchini Bangladesh.