Ofisi ya Rais wa Nigeria imetangaza kuwa kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram limewaachia huru wanafunzi wa kike 82 miongoni mwa wasichana zaidi ya 200 waliokuwa wamewateka nyara katika mji wa kaskazini mashariki mwa nchi hiyo wa Chibok mwaka 2014, mkabala wa kuachiwa huru wafungwa wa kundi hilo.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amelitaka kundi la kigaidi la Boko Haram la nchini Nigeria kuhitimisha ukiukaji wake wa haki za watoto.
Ndege za kivita za Nigeria zimefanya mashambulizi katika maficho ya wanamgambo wa Boko Haram kaskazini mashariki mwa nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika na kuua magaidi kadhaa.
Kundi la kigaidi la Boko Haram limefanya shambulio katika kambi moja ya jeshi la Nigeria na kuwaua wanajeshi kadhaa wa nchi hiyo.
Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Kuhudumia Watoto (UNICEF) umesema kuwa, walimu 600 wameuawa katika eneo la Ziwa Chad kwenye mashambulizi ya genge la kigaidi la Boko Haram tangu mwaka 2009.
Duru za habari nchini Cameroon zimearifu kwamba, kundi la kigaidi na ukufurishaji la Boko Haram limetekeleza shambulio katika kijiji cha Mbreché, kaskazini mwa nchi hiyo na kuteka nyara wasichana kadhaa wenye umri wa miaka kati ya minane hadi 14.
Jeshi la Nigeria limefanikiwa kukomboa mamia ya mateka waliokuwa wakishikiliwa na wapiganaji wa kundi la kigaidi la Boko Haram.
Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa UNICEF umeeleza kushtushwa kwake na ongezeko la watoto wadogo kutumiwa katika hujuma za kujitolea muhanga za kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram.
Afisa mmoja wa masuala ya usalama wa Niger alisema jana kwamba, wanamgambo 57 wa genge la kigaidi la Boko Haram waliuawa Jumapili usiku katika mapigano na wanajeshi wa serikali, kusini mashariki mwa nchi hiyo.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limelaani mashambulizi ya kigaidi ya kundi la Boko Haram na Daesh (ISIS) katika eneo la Ziwa Chad, barani Afrika.