Apr 26, 2024 03:07
Jeshi la Burkina Faso limewauwa kiholela raia 223, wakiwemo watoto wachanga kadhaa na watoto wengine wengi, katika mashambulizi dhidi ya vijiji viwili vinavyotuhumiwa kushirikiana na wanamgambo wenye silaha. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya shirika la Human Rights Watch iliyotolewa jana Alhamisi.