Mar 17, 2023 02:27
Wanaharakati na wanasiasa wa Ufaransa wamemshambulia kwa maneno Mratibu wa Kamisheni ya Ulaya ya Kupambana na Chuki Dhidi ya Waislamu, Marion Lalisse, baada ya kuchapisha kipande cha video kwa lugha ya Kiarabu katika Siku ya Kimataifa ya Kupambana na Chuki Dhidi ya Uislamu, na kufikia hatua ya kumutaja kuwa ni "adui wa Ulaya na mtiifu kwa Uislamu."