-
Ethiopia yaondoa rasmi viza kwa Waafrika
Oct 27, 2018 04:04Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed jana alitangaza kuwa, kuanzia tarehe 9 mwezi ujao wa Novemba, nchi yake itawaondolea viza raia wote wa nchi za Afrika.
-
Ethiopia yapata rais wa kwanza mwanamke
Oct 25, 2018 10:25Bunge la Ethiopia limemuidhinisha mwandiplomasia wa kimataifa, Sahle-Work Zewde kuwa rais wa kwanza mwanamke wa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Ethiopia yasaini makubaliano ya amani na kundi la waasi wa Ogaden
Oct 22, 2018 23:32Ethiopia imesema kuwa imesaini makubaliano ya amani na kundi lililokuwa likipigania kujitenga la Waasi wa Harakati ya Taifa ya Ukombozi wa Ogaden (ONLF) na hivyo kuhitimisha rasmi uasi uliodumu kwa zaidi ya miongo mitatu katika mkoa wa Somalia mashariki mwa nchi hiyo.
-
Ethiopia yawaachia huru watu 1,174 waliohusishwa na machafuko ya Addis Ababa
Oct 18, 2018 12:54Serikali ya Ethiopia imetangaza habari ya kuachiwa huru mamia ya watu waliokamatwa wakati wa ghasia zilizoshuhudiwa mwezi uliopita wa Septemba katika mji mkuu, Addis Ababa.
-
Kwa mara ya kwanza, Mwislamu mwanamke ateuliwa kuwa Waziri wa Ulinzi Ethiopia
Oct 17, 2018 05:25Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed Ali amemteua mwanamke Mwislamu kuwa Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo, hii ikiwa ni mara ya kwanza kabisa katika historia ya nchi hiyo.
-
Waziri Mkuu wa Ethiopia afikia makubaliano na wanajeshi waliotaka nyongeza ya mishahara
Oct 11, 2018 04:42Abiy Ahmed Waziri Mkuu wa Ethiopia jana alifikia makubaliano na mamia kadhaa ya wanajeshi wa nchi hiyo waliofika ofisini kwake wakidai nyongeza ya mishahara; ambapo wanajeshi hao walikubaliwa kumuona Waziri Mkuu huyo.
-
Ethiopia kuanza kuwapa Waafrika viza wakishawasili nchini humo
Oct 09, 2018 03:55Rais wa Ethiopia, Mulatu Teshome amesema nchi hiyo karibuni hivi itaanza kuwapa raia wote wa bara Afrika viza mara tu watakapowasili katika nchi hiyo.
-
Zaidi ya watu elfu 70 wakimbia machafuko ya kikabila magharibi mwa Ethiopia
Oct 02, 2018 12:35Zaidi ya watu elfu 70 wamekimbia machafuko na ghasia za kikabila huko magharibi mwa Ethiopia. Machafuko hayo yanatajwa kuwa ni sehemu ya ghasia zilizoikumba Ethiopia katika siku za hivi karibuni na kuzidisha mashinikizo kwa serikali ya Waziri Mkuu wa nchi hiyo Abiy Ahmed.
-
Polisi: Watu 23 wameawa katika machafuko ya hivi karibuni nchini Ethiopia
Sep 17, 2018 23:28Polisi ya Ethiopia imetangaza kuwa, kwa akali watu 23 wameuawa katika machafuko yaliyoibuka hivi karibuni jirani na mji mkuu wa nchi hiyo Addis Ababa.
-
Viongozi wa Eritrea na Ethiopia wasaini makubaliano ya amani, uhusiano wazidi kuimarika
Sep 17, 2018 10:52Viongozi wa Ethiopia na Eritrea wametia saini makubaliano ya amani huku uhusiano wa nchi hizo mbili jirani zilizokuwa na uadui mkubwa ukizidi kuimarika siku baada ya siku.