-
Yemen wafanya maandamano ya mamilioni ya watu kuwaunga mkono Wapalestina
Aug 31, 2024 00:45Kwa mara nyingine tena mamilioni ya wananchi wa Yemen wamemiminika barabarani kulaani jinai za utawala wa Kizayuni na kuwaunga mkono wananchi wa Palestina hasa wa Ukanda wa Ghaza.
-
UN: Mripuko mpya wa Kipindupindu Sudan unahatarisha maisha ya mamia ya maelfu ya wakimbizi
Aug 24, 2024 06:24Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR limeeleza kupitia mwakilishi wake nchini Sudan Kristine Hambrouck kwamba mripuko mpya wa kipindupindu nchini Sudan, ambao ni wimbi la pili tangu vilipoanza vita miezi kumi na sita iliyopita, unahatarisha maisha ya jamii zilizolazimika kuyahama makazi yao nchini kote.
-
Askari 695 wa Israel wameangamizwa, 4,357 wamejeruhiwa tangu vilipoanza vita vya Ghaza
Aug 23, 2024 23:04Msemaji wa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel ametangaza kuwa askari 695 wa utawala huo wameangamizwa tangu jeshi la utawala huo katili lilipoanzisha vita dhidi ya wakazi wa Ukanda wa Ghaza na kupambana na vikosi vya Muqawama wa Palestina.
-
Ombi la Shirika la Haki za Binadamu la Ulaya-Mediterranean la kuwekewa vikwazo Israel
Aug 22, 2024 07:16Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Ulaya na Mediterania (The Euro-Mediterranean Human Rights Monitor-Euro-Med-) limeonya katika taarifa yake siku ya Jumatano kuhusu amri za mara kwa mara za utawala wa Kizayuni wa Israel za kuwataka Wapalestina wahame katika maeneo tofauti ya Gaza na kuzitaka nchi za dunia ziuwekee vikwazo utawala huo ghasibu na zisiuunge mkono.
-
Takwa la Waislamu wa Marekani kwa Biden la kulaani ugaidi wa kiserikali wa Israel
Aug 11, 2024 10:10Baraza la Mahusiano ya Kiislamu Marekani (CAIR) limemtaka Rais Joe Biden wa nchi hiyo ajibu na kulaani vitendo vya ugaidi wa kiserikali vinavyofanywa na utawala haramu wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran: Taasisi za kimataifa ni washirika katika jinai za utawala wa Kizayuni
Aug 11, 2024 07:57Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa taasisi za kimataifa zinashiriki katika jinai za utawala wa Kizayuni.
-
Maandamano ya kulaani jinai za Israel yaendelea kufanyika nchini Morocco
Aug 09, 2024 23:02Maelfu ya wananchi wa Morocco wamefanya maandamano katika miji mbalimbali ya nchi hiyo kuwaunga mkono wananchi wa Palestina na kulaani jinai zinazoendelea kufanywa na jeshi la Israel huko Gaza.
-
Ripoti: Israel imeiba zaidi ya miili 2,000 kutoka kwenye makaburi ya Gaza
Aug 06, 2024 08:46Vikosi vya jeshi la Israel vimeiba zaidi ya miili 2,000 iliyofukuliwa kutoka kwenye makaburi mbalimbali katika ukanda wa Gaza, huku ripoti kutoka Ofisi ya Vyombo vya Habari ya Serikali ya Gaza zikisema baadhi ya maiti zimerudishwa baada ya majeshi ya Israel "kuvunjia heshima miili" ya marehemu hao.
-
Jumuiya ya Wayahudi wa Iran yataka kulipiza kisasi baada ya Israel kumuua Haniyeh
Aug 03, 2024 22:53Jumuiya ya Wayahudi wa Iran imelaani vikali mauaji yaliyofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya kiongozi wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) Ismail Haniyeh akiwa ugenini mjini Tehran, ikitoa wito wa kulipiza kisasi dhidi ya mauaji hayo.
-
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu: Leo hii, bendera ya juu kabisa ya Uislamu iko mikononi mwa watu wa Gaza
Jul 30, 2024 08:19Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amepongeza ushujaa wa wananchi wanaodhulumiwa na wenye nguvu wa Ghaza na kusema: Leo bendera ya juu kabisa ya Uislamu iko mikononi mwa watu wa Ukanda wa Gaza.