-
Hamas yaafiki kuvunja serikali yake Ghaza kwa ajili ya Umoja wa Palestina
Sep 17, 2017 23:13Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, imekubali sharti kubwa lililowekwa na chama cha Fat'h cha Mahmoud Abbas ikiwa ni pamoja na kufanyika chaguzi za kitaifa Ukingo wa Magharibi na Ukanda wa Ghaza.
-
HAMAS yawasilisha kwa Misri mpango wa kupunguza makali ya mzingiro dhidi ya Ukanda wa Gaza
Aug 23, 2017 03:15Mjumbe mwandamizi wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema harakati hiyo imewasilisha kwa serikali ya Misri mpango wa mapendekezo kadhaa ya kupunguza makali ya mzingiro uliowekwa dhidi ya eneo la Ukanda wa Gaza.
-
Mahmoud Abbas aendelea kutoa vitisho dhidi ya Wapalestina wa Gaza
Aug 16, 2017 02:49Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina ametishia tena kuchukua hatua kali zaidi za kuwaadhibu Wapalestina wa eneo la Ukanda wa Gaza.
-
Abbas azidi kuwabinya Wapalestina, akata mitandao ya kijamii
Aug 11, 2017 03:10Katika hatua inayoonekana ni ya kuzidi kuwawekea mbinyo Wapalestina, Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina Mahmoud Abbas amepasisha dikrii ya kutaka kufungwa mara moja mitandao ya kijamii na tovuti za habari katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Ndege za Israel zashambulia Wapalestina wa Ukanda wa Gaza
Aug 09, 2017 02:50Ndege za kivita za utawala wa Kizayuni wa Israel zimeshambulia makazi ya Wapalestina wa Gaza usiku wa kuamkia leo na kujeruhi watu kadhaa.
-
Oxfam: Israel na Mamlaka ya Ndani Palestina zinahusika na mgogoro wa Ghaza
Aug 07, 2017 10:28Mwakilishi wa shirika la misaada ya kibinadamu la Oxfam huko katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu ameutaja utawala wa Kizayuni wa Israel na Mamlaka ya Ndani ya Palestina kuwa zinahusika na kushtadi mgogoro katika Ukanda wa Ghaza.
-
Vikwazo, vizuizi, uhaba, sababu tatu za hatari ya kufa wagonjwa Ukanda wa Ghaza
Jul 14, 2017 22:01Jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel zingali zinaendelea dhidi ya wakazi wa Ukanda wa Ghaza na hivi sasa jinai hizo zinawasababishia vifo vya kila namna wakazi hao waliozingirwa kila upande.
-
Haniya: Haiwezekani kutenganisha baina ya Gaza na Ukingo wa Magharibi
Jul 12, 2017 10:01Mkuu wa Idara ya Siasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) amesema kuwa, harakati hiyo iko tayari kukomesha mgawanyiko ulioko huko Palestina na kwamba eneo la Gaza kamwe halitatenganishwa na Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Ndege za Israel zawavurumishia mabomu Wapalestina Ukanda wa Ghaza
Jun 27, 2017 03:27Ndege za kivita za utawala wa Kizayuni wa Israel zimevurumisha makombora kadhaa katika Ukanda wa Ghaza wakati Wapalestina katika eneo hilo wakiwa wanasherehekea siku kuu ya Idul Fitr.
-
Mahmoud Abbas aendelea kuwakomoa Wapalestina wa Gaza; aamua kuwastaafisha askari 1,000 kwa nguvu
Jun 19, 2017 03:31Katika muendelezo wa hatua za kuwakomoa Wapalestina wa Ukanda wa Gaza, Mahmoud Abbas, Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina ameunda kamati ya usalama kwa lengo la kuwastaafisha kwa nguvu na kabla ya wakati askari elfu moja wa eneo hilo.