Nov 12, 2023 06:59
Sayyid Hassan Nasrullah, Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesema wapiganaji wa harakati hiyo ya Muqawama wa Kiislamu wameanza kutumia silaha mpya, likiwemo kombora lenye kichwa kizito katika mapigano yanayoendelea mpakani mwa Lebanon na ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu (Israel), na kuongeza kuwa wataendelea kutumia mpaka huo wenye mvutano kuishinikiza Israel.