-
Sababu za kuongezeka mvutano kati ya Qatar na nchi nyingine nne za Kiarabu
Jan 13, 2018 00:14Licha ya kupita zaidi ya miezi 7 tokea kuanza mvutano kati ya Qatar na nchi nyingine nne za Kiarabu za kundi la 3+1, si tu kwamba hakuna dalili zozote zinazoonyesha kupungua mvutano huo bali umekuwa ukiongezeka siku baada ya nyingine.
-
Qatar yaishitaki Imarati UNSC kutokana na hatua zake za kichokozi
Jan 12, 2018 00:49Mwakilishi wa Qatar katika Umoja wa Mataifa amewasilisha mashitaka kwa Baraza la Usalama la Umoja dhidi ya Imarati kutokana na hatua yake ya kichokozi ya kukiuka anga yake.
-
UN yashtushwa na ukiukwaji wa haki za binadamu Imarati
Jan 10, 2018 12:32Umoja wa Mataifa umeeleza wasiwasi wake kutokana na kushtadi uvunjwaji wa haki za binadamu katika Umoja wa Falme za Kiarabu.
-
Hila za Imarati kwa ajili ya kuanzisha kambi ya kijeshi nchini Yemen
Jan 01, 2018 00:51Mtandao wa Kifaransa wa Intelligence Oline umefichukua kuwa, hivi sasa Imarati sambamba na kubadili kisiwa cha kistratijia cha Socotra nchini Yemen kuwa eneo la kijeshi, imeazimia kuanzisha kambi yake ya kijeshi katika kisiwa hicho
-
Ansarullah kuishambulia Somaliland ikiendelea kushirikiana na UAE dhidi yake
Dec 27, 2017 03:46Harakati ya Ansarullah ya Yemen imesema ikilazimu, itaishambulia jamhuri iliyojitangazia uhuru ya Somaliland kutokana na hatua yake ya kushirikiana na Umoja wa Falme za Kiarabu dhidi ya wapiganaji wa harakati hiyo ya Houthi.
-
Tunisia yapiga marufuku ndege za UAE kutua nchini humo
Dec 25, 2017 03:17Tunisia imetangaza kupiga marufuku ndege za Shirika la Ndege la Emirates la Umoja wa Falme za Kiarabu, UAE kutua nchini humo. Uamuzi huo umechukuliwa baada ya UAE kuwapiga marufuku wanawake wa Tunisia kuingia UAE au kupitia katika ardhi ya nchi hiyo ya Ghuba ya Uajemi.
-
Baada ya kushindwa njama zao dhidi ya Qatar na Yemen, kundi la Saudia lamalizia hasira zake kwa Uturuki
Dec 20, 2017 12:54Serikali ya Uturuki imekasirishwa sana na hatua ya waziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) aliyetuma ujumbe kwenye ukurasa wake wa Twitter na kumtuhumu Rais Recep Tayyip Erdogan kuwa ni kutoka kizazi cha Waturuki waliofanya wizi mjini Madina na kukandamiza Waarabu wakati wa utawala wa Uthmaniyyah (Ottoman Empire).
-
Imarati yakerwa na kuwasilishwa kesi dhidi yake ICC, yailaumu Qatar
Nov 29, 2017 04:42Waziri wa Mambo ya Nje wa Umoja wa Falme za Kiarabu ameeleza kughadhibishwa kwa Imarati na hatua ya shirika moja la kutetea haki za binadamu kufungua faili la jinai za kivita za nchi hiyo dhidi ya Yemen.
-
Faili la jinai za Imarati dhidi ya Yemen lafunguliwa ICC
Nov 28, 2017 04:14Shirika moja la kutetea haki za binadamu limewasilisha kesi katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC, likiituhumu nchi ya Umoja wa Falme za Kiarabu kuwa imetenda jinai za kivita ukishirikiana na Saudi Arabia dhidi ya Yemen.
-
Imarati yazitaka nchi za Ulaya zidhibiti misikiti kwa kuweka CCTV
Nov 15, 2017 04:15Waziri mmoja wa Umoja wa Falme za Kiarabu UAE ameitaka Ujerumani na nchi nyingine za Ulaya kudhibiti misikiti na makhatibu wa misikiti katika nchi zao kwa shabaha ya kuzuia uenezwaji wa misimamo mikali ya kufurutu ada.