-
Shamkhani: Mazungumzo ya Marekani yanaweza kuzaa matunda iwapo tu yataonyesha heshima, mantiki
Feb 03, 2026 08:10Afisa wa ngazi ya juu wa Iran amesema kuwa mazungumzo yajayo ya nyuklia na Marekani yanaweza kuwa na tija iwapo tu yatajiepusha na anga ya vitisho na madai yasiyo na mantiki, na kusisitiza kuwa Tehran haina nia ya kuhamisha nje ya nchi akiba yake ya urani iliyorutubishwa chini ya makubaliano yoyote.
-
Ripoti: Iran, Marekani kufanya mazungumzo ya nyuklia mjini Istanbul
Feb 03, 2026 07:53Iran na Marekani zinapanga kufanya duru mpya ya mazungumzo kuhusu mpango wa nyuklia wa Tehran.
-
'Hakuna Mmarekani atakayesalimika’: Mkuu wa Majeshi ya Iran asema vikosi vya jeshi viko tayari kulipiza kisasi
Feb 03, 2026 03:50Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameonya kuwa mahesabu yoyote ghalati ya maadui wa Jamhuri ya Kiislamu yatakabiliwa na jibu kali. Amesema kuwa Iran imejiandaa kikamilifu kwa makabiliano na kulipiza kisasi.
-
Pompeo aanika nafasi ya US katika ghasia za karibuni nchini Iran
Feb 03, 2026 03:11Mkurugenzi wa zamani wa Shirika la Ujasusi la Marekani CIA, Mike Pompeo, amekiri kwamba, Washington ilikuwa na mchango wa moja kwa moja katika ghasia za hivi karibuni nchini Iran, akisema Marekani "iliwasaidia moja kwa moja" wafanya fujo.
-
Iran yatahadharisha: Uvamizi wowote utakuwa na madhara makubwa kwa eneo zima la Asia Magharibi
Feb 02, 2026 14:05Iran imesema kuwa nchi za kikanda zinafanya juhudi za pamoja ili kuzuia vita kwa vile zinaelewa vyema kwamba hatua yoyote ya kijuba dhidi ya Tehran itakuwa na madhara makubwa kwa eneo zima.
-
Iran yatambua majeshi ya Ulaya kama mashirika ya kigaidi
Feb 01, 2026 10:21Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran), Mohamad Bagher Ghalibaf amelitaja Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) kama taasisi ya kipekee zaidi ya kupambana na ugaidi duniani, akibainisha kuwa Ulaya 'imejipiga risasi mguuni' kwa kuiweka IRGC kwenye orodha yake nyeusi.
-
Majasusi wa Magharibi: Iran haiundi silaha za nyuklia
Feb 01, 2026 09:41Mashirika ya ujasusi ya nchi za Magharibi yamesema hakuna dalili yoyote inayoashiria kwamba Iran inarutubisha urani kwa ajili ya "kufikia kiwango cha mabomu," gazeti la New York Times limeripoti, likinukuu vyanzo mbali mbali.
-
Iran: IRGC inadumisha amani, utulivu; uingiliaji unachochea taharuki
Feb 01, 2026 07:01Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi amesema Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) lina jukumu muhimu katika kudumisha amani na utulivu katika eneo la Ghuba ya Uajemi na Lango Bahari la Hormuz, huku akionya kwamba uwepo na vikosi vya kigeni katika eneo la Asia Magharibi umepelekea kuongezeka taharuki badala ya kupunguza mvutano.
-
Sera za uadui za Umoja wa Ulaya dhidi ya Iran; Brussels inataka nini?
Jan 31, 2026 08:57Umoja wa Ulaya umeendeleza msimamo wake wa kuingilia masuala ya ndani ya Iran kwa kuweka vikwazo vipya dhidi ya Tehran kwa kisingizio cha masuala ya haki za binadamu.
-
Ushirikiano wa Starmer na Trump; madai mapya dhidi ya mpango wa nyuklia wa amani wa Iran
Jan 31, 2026 03:34Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer ametoa tuhuma zisizo na msingi dhidi ya mpango wa nyuklia wa amani wa Iran.