-
Bloomberg: Vikwazo vya Marekani vimefali, uchumi wa Iran unaimarika
Oct 26, 2019 23:09Jarida la kimataifa la biashara la Bloomberg limethibitisha kuwa vikwazo vya Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran vimefeli na kwamba uchumi wa nchi hii karibuni utaanza kuimarika.
-
Sisitizo la Trump la kushadidisha makali katika vikwazo vya mafuta dhidi ya Iran
Oct 26, 2019 08:32Vikwazo vya nyuklia dhidi ya Iran vilitekelezwa katika marhala mbili yaani mwezi Agosti na Novemba mwaka jana baada ya Trump kutangaza kabla yake mnamo tarehe 8 Mei kuitoa Marekani katika makubaliano hayo ya nyuklia. Vikwazo hivyo vilikuwa vya upande mmoja; na vimekiuka sheria za kimataifa likiwemo azimio nambari 2231 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Japan yataka kutekelezwa kikamilifu makubaliano ya JCPOA
Oct 24, 2019 13:11Waziri Mkuu wa Japan ametoa mwito kwa nchi zote husika kutekeleza kikamilifu makubaliano ya nyuklia ya Iran JCPOA.
-
Haki za Binadamu; mchezo mchafu wa siasa za Magharibi dhidi ya Iran
Oct 24, 2019 08:45Moja ya silaha zinazotumiwa na Magharibi katika kuamiliana na nchi zenye misimamo huru ni kutumia maudhui ya haki za binadamu; na katika hilo, mtazamo wa upande mmoja tu na wa Kimagharibi kwa maudhui hiyo katika jamii ambayo ni ya Kiislamu, inayojitawala na yenye misimamo huru ni aina mojawapo ya undumakuwili unaombatana na siasa chafu.
-
Rouhani: Maadui wanadhani watausambaratisha Mfumo wa Kiislamu kwa kuhujumu JCPOA
Oct 23, 2019 23:19Rais Hassan Rouhani amewashangaa maadui wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wanaodhani kuwa, kwa kuhujumu na kukiuka makubaliano ya nyuklia ya JCPOA watausambaratisha Mfumo wa Kiislamu hapa nchini.
-
Makeke ya Trump mbele ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
Oct 22, 2019 08:20Donald Trump Rais wa Marekani mwenye kubwabwaja sana tangu aingie ikulu ya White House amechukua mkondo wa sera za chuki na uhasama dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na utendaji wake umejikita katika mashinikizo ya kiwango cha juu kabisa dhidi ya Tehran ili kwa njia hiyo aweze kulifanya taifa hili lisalimu amri na kukubali matakwa ya Washington.
-
Zarif: Ugaidi wa kiuchumi wa Marekani umeshindwa kuzima ndoto za vijana wa Iran
Oct 22, 2019 04:44Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema mashinikizo, vikwazo na ugaidi wa kiuchumi wa Marekani umeshindwa kuzima ndoto na mafanikio ya vijana wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Larijani: Iran imeandaa mazingira kwa ajili ya Afrika Kusini kuwekeza nchini
Oct 22, 2019 00:38Spika wa Majilisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema mchakato wa kuandaa mazingira kwa ajili ya Afrika Kusini kuwekeza hapa nchini umekamilika na kusisitiza kwamba, uhusiano wa pande mbili unahitaji kupigwa jeki katika ushirikiano wa kiuchumi.
-
Jeshi la Marekani linawahamisha magaidi wa ISIS kutoka Syria hadi Iraq
Oct 21, 2019 04:42Jeshi la Marekani linawabeba mamia ya magaidi wakufurishaji wa ISIS (Daesh) kutoka jangwa la al-Jazira kaskazini mashariki mwa mkoa wa Hasakah Syria na kuwaingiza katika nchi jirani ya Iraq.
-
Iran inajitegemea kikamilifu katika sekta ya nyuklia
Oct 21, 2019 04:18Jamhuri ya Kiislamu ya Iran hivi sasa inajitegemea kikamilifu katika shughuli zake za nyuklia na haipokei msaada wowote wa kigeni katika uga huo.