Jun 24, 2016 14:44
Mahakama Kuu mjini Pretoria nchini Afrika Kusini imetupilia mbali rufaa ya Rais Jacob Zuma wa nchi hiyo ya kupinga kufufuliwa kesi za ufisadi wa kifedha dhidi yake, hatua ambayo ni pigo kwa rais huyo ambaye anakabiliwa na mashinikizo ya kujiuzulu kutoka viongozi wa upinzani.