Aug 26, 2019 13:28
Mohammad Javad Zarif, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Jumapili alasiri alielekea Ufaransa katika safari ambayo haikuwa imetaraijiwa kufuatia mwaliko wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa Jean-Yves Le Drian kwa lengo la kuendelea na mazungumzo kuhusu ubunifu wa hivi karibuni wa marais wa Iran na Ufaransa kuhusu mapatano ya nyuklia ya JCPOA.