Jan 21, 2024 03:33
Rais Ebrahim Raisi wa Iran amelaani vikali shambulizi la kigaidi la Israel katika mji mkuu wa Syria, Damascus lililopelekea kuuawa shahidi washauri watano wa kijeshi wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) na kusisitiza kuwa, vitendo vya aina hiyo vya kioga haviwezi kupita hivi hivi bila kupewa jibu.