-
Frangieh: Marekani haina uwezo wa kuidhoofisha Hizbullah
May 27, 2016 23:17Mkuu wa harakati ya el Marada ya Lebanon amesema kuwa, vikwazo vya kifedha vilivyowekwa na Marekani dhidi ya Hizbullah haviwezi kuidhoofisha harakati hiyo ya muqawama wa Kiislamu.
-
Sayyid Nasrullah: Israel ingali tishio kuu kwa eneo la M/Kati
May 25, 2016 11:58Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema utawala wa Kizayuni wa Israel ndio tishio kuu kwa usalama na amani ya eneo hili.
-
Sheikh Naeem Qassim: Muqwama wa Lebanon umejiweka tayari kukabiliana na Israel
May 25, 2016 03:01Naibu Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesisitiza kuwa harakati hiyo ya muqawama iko tayari kikamilifu kukabiliana na vitisho na uvamizi unaoweza kufanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Nasrallah ampongeza kamanda wa Hizbullah aliyeuawa Syria
May 20, 2016 23:25Kiongozi wa Harakati ya Hizbullah Sayyed Hassan Nasrallah amempongeza kamanda mwandamizi wa harakati hiyo ya muqawama, Shahidi Mustafa Badreddine aliyeuawa Syria wiki jana na kusema alikuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya Israel.
-
Nabih Berri apendekeza mpango wa kuinasua Lebanon kwenye mkwamo wa kisiasa
May 19, 2016 23:36Spika wa Bunge la Lebanon amependekeza mpango wa vipengee vitatu kwa lengo la kuinasua nchi hiyo kwenye mkwamo wa kisiasa wa kubaki bila ya kuwa na Rais kwa takribani miaka miwili sasa.
-
Hizbullah yapongeza juhudi za Iran za kusuluhisha matatizo ya eneo
May 16, 2016 02:19Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amepongeza sera za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kupambana na ugaidi sambamba na jitada zake za kuzipatia ufumbuzi changamoto zinazolikabili eneo hili la Mashariki ya Kati.
-
Iran: Mgogoro wa Syria utamalizwa kwa kura za wananchi
May 14, 2016 23:22Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, mgogoro wa Syria utamalizwa kwa kura na matakwa ya wananchi wenyewe wa Syria.
-
Hizbullah yachunguza namna alivyouawa kamanda wake
May 13, 2016 03:17Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Lebanon ya Hizbullah imesema imeanzisha uchunguzi kubaini namna kamanda wake mwandamizi alivyouawa katika kile kilichotajwa kuwa hujuma ya jeshi la utawala haramu wa Israel.
-
Hizbullah: Saudia inaiunga mkono Israel kukalia kwa mabavu Palestina
May 06, 2016 08:38Afisa mwandamizi wa harakati ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon amelaani kile alichokitaja kuwa juhudi za utawala wa Aal-Saud za kukwamisha muqawama wa Wapalestina dhidi ya utawala haramu wa Israel na kusisitiza kuwa serikali ya Saudi Arabia inaunga mkono hatua ya utawala huo wa Kizayuni kukalia kwa mabavu ardhi za Palestina.
-
Saudia inawahudumia bure Wazayuni
Mar 28, 2016 23:53Sheikh Suhail Habli, mwanazoni wa Kisuni wa nchini Lebanon amezikosoa siasa za watawala wa Aal Saud na kusema kuwa, Saudi Arabia ni mfanyakazi wa bure wa Wazayuni.