-
Walibya waandamana wakipinga kukubaliwa Saiful Islam Gaddafi kugombea urais
Nov 15, 2021 23:04Raia wa maeneo ya magharibi mwa Libya wamefunga vituo vya kupigia kura wakipinga hatua ya mwana wa kiume wa kiongozi wa zamani wa Libya, Saiful Islam Gaddafi ya kuwania kiti cha urais katika uchaguzi ujao nchini humo.
-
Mkutano wa Paris wataka askari wa kigeni walioivamia Libya waondoke nchini humo
Nov 13, 2021 08:06Washiriki wa mkutano wa Paris, mji mkuu wa Ufaransa wametaka kufanyike uchaguzi katika tarehe iliyopangwa nchini Libya, kama ambavyo wamehimiza pia wajibu wa kutoka wanajeshi wa kigeni nchini humo.
-
Haftar aafiki kutimuliwa mamluki 300 wa kigeni nchini Libya
Nov 12, 2021 04:22Wawakilishi wa Jenerali mstaafu Khalifa Haftar katika kamati ya kijeshi inayojulikana kwa jina la kundi la 5+5 huko Libya wamesema kuwa wameafiki kuondolewa wapiganaji mamluki 300 wa kigeni katika maeneo yanayodhibitiwa la kundi la linalojiiita Jeshi la Taifa la Libya.
-
Kuanza zoezi la uandikishaji wa wagombea Urais na Ubunge katika uchaguzi wa Libya
Nov 09, 2021 04:17Hatimaye baada ya miezi kadhaa ya mazungumzo na vuta nikuvute baina ya makundi na mirengo tofauti ya kisiasa nchini Libya, uandikishaji majina ya wagombea wa kiti cha urais na Bunge ulianza Jumatatu ya jana tarehe 8 Novemba.
-
Libya yapinga kusimamishwa kazi Waziri wa Mambo ya Nje kabla ya uchaguzi
Nov 07, 2021 23:14Serikali ya Libya imepinga uamuzi wa Baraza la Rais la nchi hiyo wa kumsimamisha kazi Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika, wiki chache kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu.
-
UN: Watoto, wanawake 1,000 wanaozuiliwa Libya wapo hatarini
Oct 13, 2021 09:28Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa (Unicef) umetadharisha kuhusu hali mbaya inayowakabili watoto wadogo na wanawake wapatao elfu moja ambao ni miongoni mwa maelfu ya wahajiri wanaozuiliwa katika kambi za wakimbizi za kuogofya huko Tripoli, mji mkuu wa Libya.
-
Ufaransa yakiri makosa yake ya kushiriki katika mashambulio ya Libya
Oct 10, 2021 22:58Akizungumza karibuni katika mji wa Montpellier na viongozi wa nchi za Kiafrika za eneo la Sahel, Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa amekiri kwamba nchi yake ilifanya makosa kwa kushiriki katika mashambulio ya kijeshi yaliyofanyika dhidi ya Libya nwaka 2011.
-
Maiti 17 za wahajiri zapatikana ufukweni magharibi mwa Libya
Oct 06, 2021 09:31Shirika la Hilali Nyekundu la Libya limesema maiti 17 za wahajiri wanaoaminika kufa maji baada ya boti waliokuwa wakisafiria kuzama zimepatikana katika pwani ya magharibi ya nchi hiyo.
-
Bunge la Libya lapiga kura ya kutokuwa na imani na Baraza Kuu la Serikali ya nchi hiyo
Sep 23, 2021 00:43Bunge la Libya limepiga kura ya kutokuwa na imani na Baraza Kuu la Serikali ya nchi hiyo. Hatua hiyo imecukuliwa huku pande zote zinazozozana nchini Libya zikiwa mbioni kutayarisha mazingira mwafaka ya kuitisha uchaguzi huru na wa haki nchini humo na kukomesha mgogoro unaoendelea kwa zaidi ya miaka 10 sasa katika nchi hiyo ya Kaskazini mwa Afrika.
-
Bunge la Libya limepiga kura ya kutokuwa na imani na serikali ya mpito ya nchi hiyo
Sep 21, 2021 23:52Abdallah Bilhaq Msemaji wa bunge la Libya lenya makao yake katika mji wa Tobruk mashariki mwa nchi hiyo jana adhuhuri alitangaza kuwa bunge hilo limepiga kura ya kutokuwa na imani na serikali ya mpito ya hiyo.