-
Guterres aeleza wasiwasi wake kuhusu hali ya wahamiaji haramu huko Libya
Jul 27, 2019 02:43Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema kuwa amehuzunishwa sana kusikia taarifa ya kuaga dunia wahamiaji na wakimbizi wapatao 150 baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kuzama katika pwani ya Libya juzi Alhamisi.
-
Mapigano yashtadi kusini mwa Tripoli mji mkuu wa Libya
Jul 25, 2019 06:46Mapigano kati ya wanamgambo kwa jina la jeshi la kitaifa la Libya na vikosi vya serikali ya umoja wa kitaifa ya Libya yamepamba moto katika eneo la al Ramla kusini mwa Tripoli mji mkuu wa nchi hiyo.
-
Wanamgambo wa Haftar watungua droni ya Uturuki huko Libya
Jul 21, 2019 22:03Duru zenye mfungamano na wanamgambo wanaojiita jeshi la kitaifa la Libya wanaoongozwa na kamanda Khalifa Haftar zimeripoti kuwa wanamgambo hao wametungua droni ya Uturuki katika anga ya mji mkuu wa Libya, Tripoli.
-
UNHCR: Mapigano Libya yamefanya watu 120,000 wakimbie makazi yao
Jul 18, 2019 06:57Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR limesema watu zaidi ya 120,000 wamelazimika kuwa wakimbizi wa ndani kutokana na mapigano huko Tripoli mji mkuu wa Libya na viunga vyake.
-
Libya: Kudai Haftar kwamba ataanzisha mashambulio mapya ni vitisho vya kutumia vyombo vya habari
Jul 15, 2019 02:45Msemaji wa vikosi vya serikali ya mapatano ya kitaifa ya Libya amesema, vitisho vilivyotolewa na vikosi vya mashariki mwa nchi hiyo vinavyoongozwa na Khalifa Haftar kwamba vitaanzisha mashambulio mapya dhidi ya mji mkuu Tripoli ni uogofyaji na uenezaji hofu kwa kutumia vyombo vya habari.
-
Kiongozi mmoja wa Daesh aangamizwa nchini Libya
Jul 13, 2019 21:49Kiongozi mmoja wa genge la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) ameangamizwa katika shambulizi la anga wapiganaji wanaoijiita Jeshi la Taifa la Libya wanaoongozwa na Jenerali Khalifa Haftar.
-
HRW, Amnesty zataka kufungwa vituo vya kuwazuilia wahajiri Libya
Jul 12, 2019 10:48Mashirika ya kutetea haki za binadamu ya Human Rights Watch, Amnesty International na Baraza la Ulaya la Wakimbizi na Wahajiri (ECRE) yametoa mwito wa kufungwa kambi za kuwazuilia wakimbizi na wahajiri nchini Libya.
-
Kansela wa Ujerumani asisitizia ulazima wa kuacha kuiuzia silaha Libya
Jul 10, 2019 23:31Kansela wa Ujerumani Angela Merkel amesisitiza kupatikana njia ya kidiplomasia kwa ajili ya kuutatua mgogoro wa Libya na kuitolea wito jamii ya kimataifa kuacha kuiuzia silaha nchi hiyo.
-
Umoja wa Afrika walaani uingiliaji wa kigeni katika masuala ya ndani ya Libya
Jul 08, 2019 22:02Baraza la Usalama la Amani la Umoja wa Afrika limelaani vikali uingiliaji wa kigeni katika masuala ya ndani ya Libya.
-
14 wauawa katika mapigano Tripoli, mji mkuu wa Libya
Jul 07, 2019 09:05Maafisa jeshi wa Libya wamearifu kuwa watu 14 wameuawa katika mapigano huko Tripoli mji mkuu wa nchi hiyo.