-
Wahajiri zaidi ya 100 watoroka kambi za wafanyamagendo ya binadamu nchini Libya
May 26, 2018 22:04Duru za Libya zimetangaza kuwa wahajiri zaidi ya 100 wametoroka kwenye kambi kadhaa zinazodhibitiwa na wafanyamagendo ya binadamu katika mji wa Bani Walid magharibi mwa nchi hiyo.
-
Wahajiri 1,500 waokolewa katika bahari ya Mediterranean
May 26, 2018 03:23Takriban wahajiri 1,500 wamenusuriwa wakiwa katika safari hatarishi katika bahari ya Mediterranean, kwenye operesheni zilizofanyika siku ya Alkhamisi na jana Ijumaa.
-
Shambulio la bomu Benghazi, Libya laua watu saba
May 25, 2018 02:25Kwa akali watu saba wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya gari lililokuwa limesheheni mabomu kuripuka katika barabara yenye shughuli nyingi mjini Benghazi, mashariki mwa Libya.
-
Jenerali Khalifa Haftar ahimiza kuendelea mapambano dhidi ya magaidi Libya
May 23, 2018 09:26Mkuu wa vikosi vinavyoitwa Jeshi la Taifa la Libya amesema kuwa jeshi hilo litaendelea na operesheni zake za kupambana na magaidi katika mji wa Derna wa mashariki mwa nchi hiyo.
-
Watu wanne wauawa, kujeruhiwa katika shambulizi la kigaidi nchini Libya
May 22, 2018 23:12Kwa akali watu wawili wameuawa na wengine wawili kujeruhiwa kufuatia shambulizi la bomu lililotekelezwa na kundi moja la kigaidi katika mji wa Ajdabia, mashariki mwa Libya.
-
Jeshi la Libya latangaza kulitia mbaroni kundi linalomuunga mkono Kanali Muammar Gaddafi
May 21, 2018 09:30Kundi lenye mafungamano na Baraza la Kuu la Serikali ya Maridhiano ya Kitaifa nchini Libya, limetangaza kuwatia mbaroni wanachama wanaouunga mkono utawala wa Kanali Muammar Gaddafi, kiongozi wa zamani wa nchi hiyo.
-
Mashambulizi dhidi ya maeneo ya magaidi yanaendelea nchini Libya
May 20, 2018 22:03Jeshi la taifa la Libya limetangaza kuwa, limeshambulia maficho kadhaa ya magaidi katika mji wa Derna wa mashariki mwa nchi hiyo.
-
Makumi ya maelfu wahajiri haramu wa Ghana wakwama nchini Libya
May 20, 2018 10:09Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia masuala ya wakimbizi nchini Libya amesema kuwa, kuna makumi ya maelfu ya wahajiri haramu wa Ghana waliokwama nchini Libya.
-
Hatua za kiusalama zachukuliwa kukabiliana na genge la Daesh nchini Libya
May 19, 2018 09:25Viongozi wa serikali ya Libya wametangaza kuchukua hatua zaidi za kiusalama kwa ajili ya kukabiliana na kundi la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) ndani ya nchi hiyo.
-
Trump: Huenda kiongozi wa Korea Kaskazini akapatwa na hatima kama ya Gaddafi
May 18, 2018 23:43Rais Donald Trump wa Marekani amemuonya kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un kuwa huenda akapatwa na hatima kama iliyomfika kiongozi wa zamani wa Libya, Kanali Muammar Gaddafi, iwapo Pyongyang haitaachana na mradi wake wa silaha za nyuklia.