Waziri Mkuu wa Uingereza ametoa wito wa kuzidishwa ulinzi wa misikiti ya Waislamu baada ya gaidi kushambulia Waislamu waliokuwa wamekamilisha ibada ya Swala mjini London.
Kwa akali mtu mmoja ameuawa na wengine 10 wamejeruhiwa katika shambulio la kigaidi lililowalenga Waislamu waliokuwa wanatoka msikitini usiku wa kuamkia leo katika eneo la Bustani ya Finsbury kaskazini mwa mji mkuu wa Uingereza, London.
Kufuatia tukio la kuteketea moto jengo kongwe mjini London, wakazi wa mji huo wameitaka serikali ya Uingereza kutaja chanzo cha moto huo ambao umesababisha hasara kubwa ya mali na roho.
Watu wasiopungua saba wameuawa na wengine kadhaa kujruhiwa kufuatia shambulio la kigaidi lililotokea katika mji mkuu wa Uingereza London.
Rais Mohamed Abdullahi Mohamed wa Somalia ameiuomba jamii ya kimataifa iisaidie nchi yake katika kupambana na ugaidi, ufisadi na umaskini wa kuchupa mipaka; mambo ambayo amesema ndiye adui mkuu wa nchi hiyo.
Mamia ya Waislamu nchini Uingereza wamefanya maandamano katika mji mkuu London kulaani ukaliaji wa mabavu na upanuzi wa vitongoji vya walowezi za Kiyahudi katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu.
Ahmed al-Asiri, mshauri wa Wizara ya Ulinzi ya Saudia na msemaji wa muungano vamizi wa Saudia dhidi ya Yemen, ameshambuliwa na waandamanaji wanaopinga hujuma za utawala wa Aal-Saud nchini Yemen na kupigwa mayai mabovu.
Polisi ya Uingereza imetangaza kuwa mtu aliyehusika na shambulio la Jumatano kwenye kitovu cha mji mkuu wa nchi hiyo, London ni Khalid Masood mwenye umri wa miaka 52 ambaye ni mzaliwa wa Uingereza.
Kundi la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) limetangaza kuhusika katika hujuma ya kigaidi nchini Uingereza ambayo limepelekea kwa akali watu watano kuuawa na wengine 40 kujeruhiwa.
Watu watano wameuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa baada ya mtu mmoja kushambulia watu waliokuwa wakitembea kwa miguu kwa kuwagonga kwa gari nje kidogo ya jengo la Bunge la Uingireza mjini London.