-
Baada ya mgomo, sasa walimu Tunisia wafanya maandamano
Feb 07, 2019 11:10Maelfu ya walimu nchini Tunisia wamemiminika mabarabarani katika mji mkuu Tunis kushiriki maandamano yaliyoitishwa kwa lengo la kuishinikiza serikali iliyokataa kuwapandishia mishahara wafanyakazi wa umma.
-
Wayahudi wenye asili ya Ethiopia waandamana Tel Aviv kupinga ukatili wa polisi wa Kizayuni
Jan 31, 2019 11:20Maelfu ya Wayahudi wenye asili ya Ethiopia yaani Mafalasha wamefanya maandamano huko Tel Aviv kupinga ubaguzi wa rangi na ukandamizaji wa polisi wa utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Vyombo vya usalama Sudan vyamwachia huru Naibu Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani
Jan 30, 2019 11:13Vyombo vya usalama vya serikali ya Sudan vimemwachia huru Naibu Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani cha Umma Mariam Sadiq al-Mahdi.
-
Kinara wa kambi ya upinzani Cameroon atiwa nguvuni
Jan 29, 2019 04:50Vyombo vya usalama vya Cameroon vimemtia nguvuni kiongozi wa chama kikuu cha upinzani baada ya maandamano ya mwishoni mwa wiki iliyopita yaliyotawanywa na askari usalama kwa kutumia risasi za moto.
-
Waislamu Nigeria washinikiza kuachiwa huru mwanahabari Marzieh Hashemi
Jan 22, 2019 04:26Waislamu na wanaharakati wa kutetea haki za binadamu nchini Nigeria wamefanya maandamano kulaani kukamatwa na kuwekwa kizuizini nchini Marekani Marzieh Hashemi, mwandishi wa habari na mtangazaji wa kanali ya kimataifa ya Press TV ya Iran.
-
Waandamanaji waendelea kuuawa Sudan, serikali yavituhumu vyama vya mrengo wa kushoto
Jan 21, 2019 23:52Idadi ya watu waliouawa kwa kupigwa risasi nchini Sudan katika "Maandamano ya Mkate" inaendelea kuongezeka baada ya kufariki dunia mwanafunzi wa chuo kikuu aliyepigwa risasi kichwani.
-
Maelfu ya wanawake waandamana dhidi ya Trump Marekani na Ulaya
Jan 20, 2019 04:13Maelfu ya wanawake wameshiriki maandamano katika miji mikubwa ya Marekani na Ulaya kupinga sera za kibaguzi za Rais Donald Trump.
-
Wasudan waendeleza maandamano ya mkate, polisi yaua watu watatu
Jan 18, 2019 12:35Maandamano ya kumtaka Rais Omar Hassan al Bashir wa Sudan ang'atuke madarakani yameendelea mapema leo Ijumaa katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo baada ya mauaji ya watu watatu waliopigwa risasi na polisi katika maandamano ya jana mjini Khartoum.
-
Wasudan waendeleza maandamano ya mkate, wamtaka al Bashir ang'atuke
Jan 18, 2019 00:23Maelfu ya Wasudan waliandamana tena jana Alkhamisi katika miji mbalimbali ya nchi hiyo wakitaka kuondoka madarakani serikali ya Rais Omar al Bashir wa nchi hiyo.
-
Mgomo wa nchi nzima wa wafanyakazi waanza nchini Tunisia
Jan 17, 2019 04:10Muungano mkubwa zaidi wa wafanyakazi nchini Tunisia UGTT umesema mgomo wa nchi nzima wa malaki ya watumishi wa umma umeng'oa nanga hii leo Alkhamisi.