Katika hali ambayo siku nne zimepita tokea kufanyika vikao vya Makka lakini bado matokeo mabaya na hata yaliyo kinyume na matarajio ya waandaaji wa vikao hivyo yangali yanaendelea kuakisiwa kieneo na kimataifa.
Katika siku za Alhamisi na Ijumaa, Saudi Arabia iliandaa vikao vitatu katika mji mtakatifu wa Makka. Vikao hivyo vilikuwa vya kuhudumia ajinabi na maadui wa umma wa Kiislamu na wakati huo huo vimebainisha wazi kuchanganikiwa na kupoteza mwelekeo watawala wa nchi hiyo.
Amir wa Qatar amekataa ombi la mfalme wa Saudi Arabia la kufanya safari katika mji wa Makka na badala yake amemtuma Waziri wake Mkuu kumwakilisha huko Saudia.
Wairani 85,200 wanatazamiwa kwenda nchini Saudi Arabia kutekeleza ibada tukufu ya Hija mwaka huu.
Wasomi wakubwa wa Kiislamu nchini Nepal wameulaani utawala wa kifalme wa Aal-Saud nchini Saudia kwa hatua yake ya kutumia kisiasa na kwa malengo yao binafsi ibada ya Hijjah na maeneo matukufu ya Waislamu.
Malaysia imetangaza habari ya kuanzishwa bodi ya kimataifa ya kuchunguza na kusimamia idara na uendeshaji wa Saudi Arabia katika maeneo matakatifu ya Makka na Madina na vilevile kulinda maeneo na turathi za kihistoria.
Kiongozi wa kiroho wa Wakristo wa Palestina Kasisi Manuel Musallam amesema, hatua iliyochukua Marekani hivi karibuni dhidi ya Quds inalenga kuanzisha vita vya kidini ambavyo vitafika mpaka Makka.
Mamia ya mahujaji wamenusurika katika ajali ya moto uliotokea katika jengo la ghorofa 15 mjini Makkah, Saudi Arabia.
Hivi karibuni Wizara ya Mambo ya Nje ya Iraq ilitoa jibu dhidi ya matamshi ya Thamer Al-Sabhan, Waziri Mshauri wa Saudia katika masuala ya nchi za Ghuba ya Uajemi, ikisema kuwa wizara hiyo ya kigeni ya Iraq ni mali ya Wairaq wote.
Maulama wa Kiislamu nchini Yemen wamekadhibisha madai yaliyotolewa na utawala wa kifalme wa Saudi Arabia uliosema jeshi na wapiganaji wa Yemen wameshambulia mji mtakatifu wa Makka.