-
Jerusalem Post: Israel imeshtushwa na kasi ya Iran ya kujiimarisha upya kijeshi
Aug 15, 2026 03:53Gazeti la kizayuni la Jerusalem Post limefichua kuwa, maafisa wa ulinzi wa Israel wameshtushwa na namna Iran ilivyojenga upya na kwa kasi uwezo wake wa kijeshi tangu baada ya mashambulizi makali ya Marekani na utawala huo wa kizayuni wakati wa kipindi cha mwanzoni mwa vita vya kichokozi vilivyoanzishwa na tawala mbili hizo dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Ripoti: Iran inadhihirisha uwezo unaoongezeka wa kushambulia shabaha za kijeshi za US kupitia operesheni za pamoja
Jul 29, 2026 02:59Iran imeonyesha uwezo unaoongezeka wa kushambulia vituo vya kijeshi vya Marekani kote Asia Magharibi kwa kuchanganya ndege zisizo na rubani za mashambulizi na makombora ya kisasa ya balestiki. Hii ni kwa mujibu wa ripoti iliyomnukuu ripoti afisa wa ngazi ya juu wa Marekani.
-
IRGC yashambulia kambi za Marekani huko Kuwait, Bahrain baada ya mashambulizi ya ndege zisizo na rubani katika ardhi ya Iran
Jun 06, 2026 11:24Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuwa limeshambulia kambi mbili za anga za Marekani huko Kuwait na vituo vilivyobaki vya Kikosi cha Tano cha Marekani (US Fifth Fleet) huko Bahrain ili kujibu uchokozi wa hivi karibuni wa Marekani.
-
IRGC: Tumewavurumishia maadui makombora 700, droni 3,600 mpaka sasa
Mar 17, 2026 03:38Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) limesema limepiga shabaha za Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel kwa makombora zaidi ya 700 na ndege zisizo na rubani 3,600 tangu Jamhuri ya Kiislamu ianzishe operesheni za kulipiza kisasi cha mashambulizi ya kichokozi ya maadui hao mwishoni mwa Februari mwaka huu.
-
Jen. Mousavi: Iran imeivurumishia Israel makombora 30 ya balestiki
Mar 14, 2026 03:48Kamanda wa Kikosi cha Anga za Mbali cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran IRGC amesema asilimia kubwa ya makombora 30 ya balestiki yaliyovumishwa na Jamhuri ya Kiislamu usiku wa Lailatul Qadr yalipiga shabaha zilizokusudiwa kwa usahihi mkubwa.
-
Nini maana ya Marekani kushindwa kistratejia?
Mar 09, 2026 09:02Kwa nini Marekani inakaribia kushindwa kistratejia? Jibu la swali hili linapatika katika utambulisho wa vita vya sasa vilivyoanzishwa na Marekani na Israel dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Meja Jenerali Mousavi: Tumeimarisha uwezo wa makombora yetu
Feb 05, 2026 23:26Afisa mwandamizi wa Jeshi wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu imeimarisha mifumo yake ya kujilinda kwa kuboresha makombora ya balestiki yaliyotengenezwa ndani ya nchi.
-
"Uwezo wa makombora ya Iran umeimarika, tayari kukabili adui"
Dec 23, 2025 23:10Msemaji wa Jeshi la Iran amesema kwamba, uwezo wa vikosi vya majini, ardhini, na makombora vya Jamhuri ya Kiislamu viko tayari kikamilifu kukabiliana na senario yoyote tarajiwa ya adui, akisisitiza kwamba Tehran bado haijatumia nguvu yake halisi ya makombora.
-
Iran yazindua makombora ya Emad, Ghadr yaliyoboreshwa
Oct 19, 2025 03:06Kikosi cha Wanaanga cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) kimezindua makombora yaliyoboreshwa ya Emad na Ghadr katika miji ya makombora ya chini ya ardhi.
-
Mji wa Bat Yam umekuwa kama Gaza baada ya mashambulizi ya makombora ya Iran dhidi ya Israel
Jun 30, 2025 07:57Gazeti la Israel la lugha ya Kiibrania limeripoti kuwa mji wa Bat Yam katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu (Israel) sasa unafanana na maeneo yaliyoathiriwa na vita ya Ukanda wa Gaza baada ya mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Iran dhidi ya utawala wa Israel.