Aug 04, 2023 12:09
Ujumbe wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS) umeondoka katika mji mkuu wa Niger, Niamey bila kukutana na kiongozi wa mapinduzi, Jenerali Abdourahmane Tchiani, huku rais aliyeondolewa madarakani, Mohamed Bazoum akitoa wito kwa jamii ya kimataifa kusaidia kurejesha utawala wa kikatiba.