-
Korea Kaskazini yavurumisha kombora la balestiki kuelekea Japan
Nov 29, 2017 04:45Korea Kaskazini imefyatua kombora jengine la balestiki lililopaa juu ya kisiwa cha Japan na linaloweza kulenga sehemu yoyote ya ardhi ya Marekani, huku ikisisitiza kuwa sasa ina uwezo kamili wa kinyuklia.
-
Kila siku wanawake 600 hufanyiwa vitendo vya ukatili nchini Marekani
Nov 27, 2017 00:29Vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya wanawake katika nchi za Magharibi na hasa Marekani vimefikia kiwango cha kutia wasiwasi kinyume na inavyodaiwa huku ikiripotiwa kwamba kila siku wanawake 600 hufanyiwa vitendo vya ukatili nchini humo.
-
Kufukuzwa wanadiplomasia, zilzala katika diplomasia ya Marekani
Nov 26, 2017 04:18Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Marekani inapanga mkakati wa kuwafukuza kazi wanadiplomasia wanawake wenye asili ya Kilatini na Kiafrika ikiwa ni katika kuendelezwa hatua za kibaguzi za serikali mpya ya Marekani.
-
Ripoti: Akhari ya mashambulizi ya kigaidi Marekani yanafanywa na Wamarekani
Nov 26, 2017 00:14Ripoti mpya iliyochapishwa hivi karibuni imebaini kuwa, asilimia 84 ya watu waliofanya mashambulizi ya kigaidi nchini Marekani ni raia wa nchi hiyo.
-
Al Bashir: Marekani ina mpango wa kuigawa Sudan
Nov 25, 2017 12:44Rais Omar al Bashir wa Sudan amesema kuwa mashinikizo na njama za Marekani ndivyo vilivyopelekea kugawanywa Sudan katika nchi mbili na kwamba Washington ina mpango wa kuigawa zaidi Sudan katika nchi tano tofauti.
-
Marekani yaongeza idadi ya wanajeshi wake kwa asilimia 33 Mashariki ya Kati
Nov 24, 2017 00:46Idadi ya wanajeshi wa Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati wameongezeka kwa asilimia 33 katika kipindi cha miezi minne iliyopita.
-
Saudia inatumia mamluki wa Marekani kuwatesa wanawafalme wanaozuiliwa
Nov 23, 2017 10:54Inaarifiwa kuwa, utawala wa Riyadh umekuwa ukiwatumia mamluki waliowakodisha kutoka Marekani katika kuwatesa na kuwakandamiza wanawafalme na wajasiriamali mabilionea wa Saudi Arabia waliokamatwa hivi karibuni katika kile kilichotajwa kuwa wimbi la vita dhidi ya ufisadi.
-
Ayatullah Khamenei: Vijana wenye imani wameipigisha magoti Marekani kwa kuiangamiza Daesh
Nov 22, 2017 13:12Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, adui amezidisha uhasama wake kwa shabaha ya kuangamiza muqawama na mapambano yaliyoanzishwa na fikra ya kimapinduzi na Kiislamu katika eneo la Mashariki ya Kati, lakini vijana na waumini wenye istiqama wamewapigisha magoti maadui na kuthibitisha tena kivitendo kaulimbiu ya "Sisi Tunaweza" kwa kuliangamiza tezi la sarati na kitakfiri la Daesh.
-
Chad yakanusha madai ya Marekani kuwa rais wake alipokea rushwa
Nov 22, 2017 12:59Serikali ya Chad imekadhibisha vikali tuhuma zilizotolewa na Marekani kwamba Rais Idriss Deby wa nchi hiyo ya Kiafrika alipokea rushwa ya dola milioni 2 za Marekani ili kutoa haki ya kustafidi na mapato ya mafuta ya nchi hiyo.
-
Ukiukaji wa makubaliano ya JCPOA na tabia ya Marekani ya kutotekeleza majukumu yake
Nov 19, 2017 13:34Mwenendo wa Marekani wa kukiuka makubaliano ya kimataifa ya nyuklia ya Iran JCPOA kwa kifupi umeingia katika awamu mpya baada ya matamshi yaliyotolewa na Rais wa nchi hiyo, Donald Trump.