-
Kwa miongo saba, Marekani imeipatia Israel msaada wa dola bilioni 300
Apr 07, 2024 03:34Jopo la wanafikra la Baraza la Uhusiano wa Nje la Marekani limetoa ripoti kuhusu kiwango cha msaada wa karibu dola bilioni 300 ambazo Washington, ikiwa ndiye muungaji mkono mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel, imetoa katika muda wa miongo saba kuupatia utawala huo.
-
Msaada mpya wa silaha wa Marekani kwa Israel wa kufanyia mauaji makubwa zaidi ya kimbari ya Wapalestina
Apr 01, 2024 07:23Sambamba na juhudi zinazofanywa kimataifa kwa lengo la kusimamisha mauaji ya kimbari ya Wapalestina yanayofanywa na utawala wa Kizayuni; na mashinikizo yanayotolewa kwa utawala huo uhakikishe unaruhusu kuingizwa misaada ya kibinadamu katika Ukanda wa Ghaza, duru za habari za Marekani zimeripoti kuwa serikali ya Washington imeidhinisha kupatiwa Israel shehena mpya ya silaha za kisasa ili kuweza kuua idadi kubwa zaidi ya Wapalestina.
-
Maandamano ya kuwaunga mkono wananchi madhulumu wa Palestina na Gaza yafanyika katika nchi mbalimbali
Mar 31, 2024 07:58Wananchi huko Italia, Norway, Marekani, Japan na Morocco kwa mara nyingine tena wameandamana kulaani mauaji ya kimbari ya raia wa Palestina yanayofanywa na wanajeshi ghasibu wa utawala wa Kizayuni huko Ukanda wa Gaza.
-
Zelensky aonya: Bila msaada wa kijeshi wa Marekani, Ukraine italazimika kurudi nyuma
Mar 30, 2024 22:47Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine amesema iwapo nchi yake haitopatiwa msaada wa kijeshi ulioahidiwa na Marekani ambao kwa sasa umezuiwa kutokana na mizozo iliyomo ndani ya Kongresi ya nchi hiyo italazimika kurudi nyuma katika vita na Russia hatua kwa hatua.
-
CDC: Maambukizi ya magonjwa ya zinaa yameongezeka sana Marekani
Mar 29, 2024 08:28Mambukizi ya magonjwa ya zinaa (STIs) yanaonekana kuongezeka kwa kiwango cha kuogofya miongoni mwa watu wazima nchini Marekani.
-
Wapalestina: Gati ya muda inayotaka kujenga Marekani Ghaza ni "Bandari ya Uvamizi"
Mar 29, 2024 03:54Wapalestina wanaielezea gati ya muda inayojengwa na Marekani kwenye pwani ya mji wa Ghaza kuwa ni "bandari ya uvamizi na ukaliaji ardhi kwa mabavu".
-
CAIR: UN ichunguze jeshi la Israel lilivyowaua Wapalestina bila sababu na kuzifukia maiti zao
Mar 28, 2024 06:39Baraza la Mahusiano ya Kiislamu Marekani [CAIR] limetoa wito kwa Umoja wa Mataifa kuchunguza video inayoonyesha wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel wakiwapiga risasi bila sababuu Wapalestina wawili wanaoonekana kuwa hawana silaha kisha kuzifukia maiti zao kwa buldoza.
-
Yemen yafanya mashambulizi 6 dhidi ya US, UK na Israel
Mar 27, 2024 04:09Vikosi vya Jeshi la Yemen vimefanya mashambulizi sita dhidi ya meli za Marekani, Uingereza na utawala haramu wa Israel, ukiwa ni muendelezo wa operesheni za kuwaunga mkono wananchi madhulumu wa Palestina na kujibu uvamizi wa Washington na London dhidi ya Yemen.
-
Moscow: EU imekiri kuwa inahudumia ubeberu wa Marekani
Mar 26, 2024 22:37Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia amesema matamshi ya karibuni ya Josep Borrell, Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya ni ungamo la Magharibi kwamba inajihusisha na mgogoro wa Ukraine ili kuisaidia Marekani kudumisha nafasi yake ya ubeberu duniani.
-
Undumakuwili wa Marekani kuhusiana na utawala wa Kizayuni na vita vya Gaza
Mar 25, 2024 22:39Marekani, ikiwa ni mshirika muhimu zaidi na muungaji mkono asiye na masharti wa utawala wa Kizayuni wa Israel, inatekeleza sera ya undumakuwili kuhusu utawala huo na jinai zake. Kwa upande mmoja, katika kitendo cha kuonyesha mshikamano na Israel, Washington imetangaza msaada mpya wa kijeshi kwa utawala huo sambamba na kukata misaada kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Wapalestina UNRWA.