Aug 19, 2021 08:00
Rais Abdelmajid Tebboune wa Algeria amesema kuwa, nchi hiyo inatazama upya uhusiano wake na nchi ya Morocco. Rais wa Algeria amesema kuwa, nchi hiyo imefikia uamuzi huo baada ya hatua za hivi karibuni za Morocco ambazo ni za chuki na hasama dhidi ya nchi yetu.